Saturday 30 January 2010

NI FAINALI!!!!!!!
Egypt v Ghana
• Jumapili, Januari 31 Novemba 11 Stadium, Luanda, Angola saa 1 usiku [bongo taimu]
Misri, Mabingwa Watetezi wa Afrika, watakuwa wakicheza Fainali yao ya 3 mfululizo huku wakiwania kuweka rekodi ya kuwa Nchi ya kwanza kutwaa Taji la Afrika mara 3 mfululizo watakapopambana na Ghana.
Katika mechi 5 za Fainali hizi, Misri wamefunga jumla ya bao 14 na wamezitoa Timu ngumu za Cameroun, kwenye Robo Fainali, na Algeria kwenye Nusu Fainali.
Ghana ni Timu inayowakilishwa na Vijana wengi na wengi hawakuipa matumaini makubwa hasa baada ya injini yao Michael Essien kuumia na kujitoa kwenye Kikosi.
Hata hivyo wakiongozwa na Chipukizi kina Andre Ayew na Asamoah Gyan, Shujaa wao aliefunga goli moja moja za ushindi Robo Fainali na Nusu Fainali walipozibwaga Angola na Nigeria.
Kwenye Kundi lao, Ghana walifungwa na Ivory Coast 3-1 na kisha wakafunga Burkina Faso 1-0.
Wadau wanategemea Wachezaji Mohamed Zidan wa Misri anaecheza Borussia Dortmund ya Ujerumani na wa Ghana Andre Ayew wa Marseille ya Ufaransa kung’ara kwa Timu zao kwenye hiyo Fainali.
Makocha wote, Milovan Rajevac wa Ghana na Hassan Shehata wa Misri, wamekataa kuzungumzia lolote kuhusu Fainali hiyo.
VIKOSI VINATEGEMEWA KUWA:
Egypt [Fomesheni 3-5-2]
El Hadhary – Gomaa, Said, Fathallah – Mohammady, Fathi, Moawad, Hassan, Abd Rabo – Metab, Zidan
Ghana [Fomesheni 4-4-2]
Kingson - Inkoom, Sarpei, Addy, Vorsah - Agyeman-Badu, Draman, Kwadwo Asamoah, Gyan - Ayew, Agyemang
BIGI MECHI Jumapili: Arsenal v Man United
Ni mechi ambayo Sir Alex Ferguson wa Manchester United ameibatiza ‘mechi kubwa kwa msimu huu’ kwa vile Arsenal na Manchester United zipo kwenye kinyang’anyiro cha Ubingwa wa Ligi Kuu wakiwafukuza vinara Chelsea, lakini Arsene Wenger yeye anaamini matokeo yake si muhimu mno kuamua nani Bingwa kwa vile kila Timu itabaki kwenye kinyang’anyiro lolote linalokuwa.
Katika mzunguko wa kwanza huko Old Trafford, Manchester United waliifunga Arsenal 2-1 lakini Manchester United hawajaishinda Arsenal ugenini kwenye Ligi Kuu tangu Februari 2005 waliposhinda 4-2 Uwanja wa zamani Highbury.
Katika mechi ya mwisho ya Ligi Kuu hapo Jumatano, Arsenal walitoka suluhu 0-0 na Aston Villa huko Villa Park na hivyo kuikosa nafasi ya kuipiku Manchester United toka nafasi ya pili na pia Chelsea na kuongoza Ligi.
Vile vile katika mechi hiyo Arsenal walipata pigo pale Difenda wao wa kutumainiwa Thomas Vermaelen kuumia na huenda asicheze mechi hii na nafasi yake pengine itachukuliwa na Mkongwe Sol Campbell.
Nao Manchester United waliifunga Hull City 4-0 kwenye mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu huku Wayne Rooney akifunga bao zote 4.
Katika mechi hii, Man U watamkosa Rio Ferdinand aliefungiwa mechi 4 kwa kosa la kumpiga Craig Fagan wa Hull lakini Difenda wao wa kutumainiwa Nemanja Vidic amepona na huenda akacheza.
VIKOSI VINATEGEMEWA KUWA:
Arsenal (Fomesheni 4-3-3): Almunia; Sagna, Gallas, Campbell, Clichy; Denilson, Fabregas, Ramsey; Rosicky, Bendtner, Arshavin.
Man United (Fomesheni 4-4-2): Van der Sar; Rafael, Brown, Evans, Evra; Valencia, Fletcher, Scholes, Giggs; Rooney, Berbatov.
Refa: Chris Foy
LIGI KUU: MATOKEO MECHI ZA Jumamosi, Januari 30
Birmingham 1 v Tottenham 1
Fulham 0 v Aston Villa 2
Hull 2 v Wolves 2
Liverpool 2 v Bolton 0
West Ham 0 v Blackburn 0
Wigan 0 v Everton 1
Burnley v Chelsea [INAANZA saa 2 na nusu usiku bongo taimu]
MECHI ZA Jumapili, 31 Januari 2010
[saa 10 na nusu jioni]
Man City v Portsmouth
[saa 1 usiku]
Arsenal v Man United

No comments:

Powered By Blogger