Saturday 30 January 2010

SKANDALI LA TERRY!!!
• Unahodha England kumtoka?
• Atajwa kortini baada ya kuitaka Mahakama isimtangaze!!
Ingawa kulikuwa na tetesi za muda mrefu kuwa John Terry, Nahodha wa Chelsea na England, ana ‘skandali’ ambalo kuna Gazeti la Uingereza limelivalia njuga na kutaka kulilipua, FA ilikataa kumvua Unahodha wa England na Mkuu wake, Ian Watmore, alikaririwa kabla ya Krismas mwaka jana kuwa uamuzi huo ni juu ya Fabio Capello, Kocha wa England.
Lakini jana skandali hilo limeingia hatua mpya pale Mahakama kuamua haioni sababu yoyote ya jina la John Terry kutotangazwa na hivyo Magazeti yakapata ‘sikukuu’ kumtaja Terry katika sakata hilo linalomhusisha kufanya uhusiano wa kimapenzi na Bibi Vanessa Perroncel aliekuwa Mpenzi wa Mchezaji mwenzake wa Chelsea wakati huo, Wayne Bridge, ambae sasa yuko Manchester City.
Wadau sasa wameshika bango wakidai ‘uhuni’ huo kwa mtu mwenye ndoa na pia Nahodha wa England unafedhehesha heshima hiyo hivyo ni bora Terry akavuliwa huo Unahodha hasa kwa vile imebaki miezi mitano kabla Fainali za Kombe la Dunia kuanza na pia England ipo mbioni kugombea kuwa Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2018.
Wengine walikumbusha na kufanananisha na skandali la kauli potofu ya aliekuwa Meneja wa England, Glenn Hoddle, alipodai vilema wamepewa adhabu na Mungu na kauli hiyo ilimkosti kazi yake alipolazimika kujiuzulu Umeneja wa England.
Watu wa karibu na Wayne Bridge wamedai Beki huyo wa Manchester City aliekuwa rafiki wa karibu mno na John Terry alichukizwa mno aliposikia uhusiano wa mpenzi wake Vanessa na John Tery hasa kwa vile wao walikuwa ni wageni waalikwa kwenye harusi ya Terry iliyofanyika mwaka 2007.

No comments:

Powered By Blogger