Wednesday 27 January 2010

Carling Cup: Leo moto kuwaka Old Trafford??
• Marudio Man United v Man City
FA imetoa onyo kali kwa Mameneja, Wachezaji na Washiriki wote wa Klabu mbili za Jiji la Manchester, Manchester United na Manchester City, kabla ya pambano lao la Jumatano Januari 27 la marudiano ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling Uwanjani Old Trafford, ili kuepusha mtafaruku kati ya Mashabiki wa Timu hizo mbili ambao ni Mahasimu wakubwa.
Katika mechi ya kwanza wiki iliyopitwa iliyochezwa nyumbani kwa Man City Uwanjani City of Manchester Wenyeji waliwafunga Man United 2-1.
Lakini katika pambano hilo kulitokea kitendo ambacho kimekuwa gumzo kubwa pale Carlos Tevez, aliekuwa Mchezaji wa Man United kabla kwenda Man City, ambae ndie aliifungia Man City bao zao 2 kwenda mbele ya benchi la Man United kila alipofunga bao kuwakejeli na mwenyewe Tevez anadai yeye alikuwa akimdhihaki Nahodha wa Man United Gary Neville aliekuwa benchi kwa kauli yake kuwa Tevez hana thamani ya Pauni Milioni 25 zilitokiwa kumbakisha Man United na ndio maana klabu hiyo haikumbakisha.
Inasemekana kejeli za Tevez zilimfanya Neville amwonyeshe Tevez ishara ya kidole kimoja ambacho wengi hutafsiri ni matusi.
Wachezaji hao wawili wamepewa onyo kali na la mwisho na FA kutorudia vitendo hivyo.
FA imeshawasiliana na Polisi wa Manchester ambao wataimarisha ulinzi na ambao watawasachi Washabiki wote watakaoingia Uwanjani kuhakikisha hawabebi silaha.
Pia imefafanunuliwa kuwa endapo mechi hiyo itamalizika huku idadi ya magoli iko sawa hadi dakika 90 zikiisha magoli ya ugenini hayatahesabiwa kama mawili na mechi itaingia muda wa nyongeza wa dakika 30 na hizo zikiisha huku idadi ya magoli ipo sawa basi hapo ndipo magoli ya ugenini yatahesabiwa kama mawili ili kumpata Mshindi.
Ikiwa pia Timu zitafungana kwa magoli hayo ya ugenini basi itapigwa mikwaju mitano ya penalti ili kumpata Mshindi atakeingia Fainali kucheza na Aston Villa aliemtoa Blackburn kwenye Nusu Fainali kwa jumla ya mabao 7-4.
Chipukizi wa Fulham kutua Man United?
Fulham inasemekana imekubali ofa ya Manchester United ya kumnunua Mlinzi Chipukizi ambae pia ni Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Vijana wa chini ya miaka 21 ya England, Chris Smalling.
Mchezaji huyo amekuwa akiwaniwa na Klabu kadhaa ikiwemo Arsenal lakini inaelekea Man United ndio itafuzu kumnyakua.
Smalling alijiunga na Fulham mwaka 2008 na alicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu tarehe 28 Desemba 2009 Fulham ilipoivaa Chelsea.
MATOKEO LIGI KUU Jumanne, Januari 26
Portsmouth 1 v West Ham 1
Tottenham 2 v Fulham 0
Wolves 0 v Liverpool 0
Bolton 1 v Burnley 0

No comments:

Powered By Blogger