Saturday 30 January 2010

LIGI KUU: Matabaka yaanza kujitokeza!
Kwenye msimamo wa Ligi Kuu kumeanza kujitokeza matabaka yanayotenganisha vikundi vya Timu na kila kikundi kinaonekana wazi kugombea kitu chao.
Kundi la kwanza ni lile la Timu 3 za juu ambazo ndizo unazoweza kusema wanawania Ubingwa.
Kundi hili linaongozwa na Chelsea wenye pointi 51 kwa mechi 22, wakifuata Mabingwa Watetezi Manchester United wenye pointi 50 kwa mechi 23 na Arsenal ni wa 3 pointi 49 kwa mechi 23 pia.
Kundi la pili ni lile linalowania nafasi ya 4 ambalo lina Timu 4 nazo ni Tottenham pointi 41 kwa mechi 23, Liverpool pointi 38 kwa mechi 23, Manchester City pointi 38 kwa mechi 21 na Aston Villa pointi 37 kwa mechi 22.
Kundi la 3 ni lile lenye Timu kama 5 ambazo zinalifukuza Kundi la pili kwa mbali kidogo na hili lina Birmingham, Everton, Fulham, Blackburn na Stoke.
Pengine unaweza ukaiingiza Sunderland humo.
Mwishowe ni lile Kundi lenye nia tu ya kujinusuru wasishushwe Daraja lakini hili lina matabaka mawili ya lile lenye afueni na lile la taaban bin hoi.
Kwenye afueni unaweza kuziweka Sunderland pointi 23 na Wigan [22].
Kwenye taabani yuko yule alieshika mkia Portsmouth mwenye pointi 14 tu na juu yake yupo Hull pointi 19 wakifuatia Burnley [20], Wolves [20], West Ham [20] na Bolton [21].
MSIMAMO LIGI KUU England: [Timu zimecheza mechi 23 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 51 [mechi 22]
2 Man Utd pointi 50
3 Arsenal pointi 49
4 Tottenham pointi 41
5 Liverpool pointi 38
6 Manchester City pointi 38 [mechi 21]
7 Aston Villa pointi 37 [mechi 22]
8 Birmingham pointi 33 [mechi 22]
9 Everton pointi 29 [mechi 22]
10 Fulham pointi 27 [mechi 22]
11 Blackburn pointi 27
12 Stoke pointi 25 [mechi 21]
13 Sunderland pointi 23 [mechi 22]
14 Wigan pointi 22 [mechi 21]
15 Bolton pointi 21 [mechi 21]
16 West Ham pointi 20 [mechi 22]
17 Wolves pointi 20 [mechi 22]
18 Burnley pointi 20 [mechi 22]
19 Hull pointi 19 [mechi 22]
20 Portsmouth pointi 14 [mechi 21]

No comments:

Powered By Blogger