Monday 25 January 2010

KWA UFUPI TU………………..
• Gerrard yuko fiti
Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard amepona maumivu yake ya musuli wa mguu na kesho huenda akaonekana dimbani kucheza mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Wolves.
Gerrard aliumia Januari 13 kwenye mechi ya Kombe la FA waliyofungwa na Reading na kutolewa nje ya mashindano hayo.
• Kinda wa Man U aenda kwa Mwana wa Fergie!!!
Danny Welbeck, miaka 19, ambae ni Straika wa Manchester United amechukuliwa kwa mkopo na Preston North End hadi mwishoni mwa Msimu huu.
Preston ipo Daraja la Championship ambalo liko chini tu ya Ligi Kuu na Meneja wao ni Mtoto wa Sir Alex Ferguson aitwae Darren Ferguson.
• Ronaldo afunga 2, alambwa Nyekundu!
Cristiano Ronaldo hapo jana alifunga bao zote 2 za ushindi wa Real Madrid dhidi ya Malaga kwenye La Liga lakini akapewa Kadi Nyekundu dakika ya 70 baada ya mkono wake kumpiga Patrick Mtiliga wa Malaga na kumvunja pua.
• Mchezaji wa Paraguay ala shaba Mexico!!
Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Paraguay anaecheza soka huko Mexico na Club America, Salvador Cabanas, miaka 29, amepigwa risasi kichwani na hali yake ni tete.
Cabanas aliwahi kuwa Mchezaji Bora wa Marekani Kusini mwaka 2007.

No comments:

Powered By Blogger