Friday 29 January 2010

Rooney: Man United si Timu ya Mtu Mmoja!!
Wayne Rooney amepinga vikali kauli za watu kadhaa akiwemo Supastaa wa zamani England Alan Shearer kwamba Manchester United sasa inamtegemea yeye peke yake ili kupata ushindi.
Rooney juzi ndie aliefunga bao la ushindi kwenye Nusu Fainali ya Kombe la Carling dhidi ya Manchester City katika mechi waliyoshinda 3-1 na hivyo kuitoa City kwa jumla ya bao 4-3 katika mechi mbili za hiyo Nusu Fainali na kuipeleka Timu yake Fainali Wembley watakapocheza na Aston Villa Februari 28.
Katika mechi ya nyuma ya hiyo, Manchester United waliishinda Hull City 4-0 kwenye Ligi Kuu na Rooney ndie aliefunga bao zote 4.
Mpaka sasa Rooney ameshafunga jumla ya mabao 21 msimu huu na kwenye Ligi Kuu yeye ndie anaeongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 19.
Rooney ametamka: “Sioni kama hii ni Timu ya mtu mmoja! Kama sipewi mipira, sifungi! Na kama sifungi, wengine watafunga tu!”

No comments:

Powered By Blogger