Saturday 30 January 2010

SAKATA LA TERRY: FA yagoma kuzungumzia kashfa!!!
Chama cha Soka England, FA, kimekataa kuzungumza lolote kuhusu Nahodha wa England John Terry kufuatia mlipuko wa taarifa zake kwenye vyombo vya habari akihusishwa na uhusiano wa kimapenzi na gelfrendi wa Mchezaji mwenzake Wayne Bridge uliotajwa jana kufuatia Mahakamani kufutilia mbali uamuzi wa awali wa jina la Terry kutotajwa katika tuhuma hizo.
Kumekuwa na wito toka kona nyingi kuwa Terry ambae ana Mke na Watoto ajiuzulu Unahodha wa England.
Klabu ya John Terry ambayo pia ni Nahodha, Chelsea, imesema ipo pamoja na Terry kwenye matatizo yake na kwamba inachukulia kashfa hiyo kama tatizo binafsi la Mchezaji huyo na wako tayari kumpa msaada pamoja na familia yake.
UHAMISHO: Dirisha kufungwa Jumatatu!!!
Dirisha la Uhamisho wa Wachezaji linategemewa kufungwa Jumatatu na, ingawa kumekuwa hamna kikubwa mno kilichofanyika kwenye kipindi hiki, zifuatazo ni taarifa na tetesi zilizotanda kwenye dakika hizi za mwisho:
-Babel
Winga huyu wa Liverpool amehusishwa na Birmingham na inasemekana ofa ya Klabu hiyo ya Pauni Milioni 9 ilikataliwa na Liverpool lakini inadaiwa majadiliano yanaendelea.
-Dindane
Aruna Dindane kutoka Ivory Coast ambae yuko Portsmouth kwa mkopo akitokea Klabu ya Ufaransa Lens huenda nae akachukuliwa na Birmingham.
-Pavlyuchenko
Roman Pavlyuchenko ni chaguo nambari wani la Birmingham ingawa Tottenham wameweka ngumu lakini mjadala unaendelea na pengine uamuzi utatoka wakati wowote.
-Wilshere
Imeshathibitishwa kuwa Bolton Wanderers imemchukua Jack Wilshere kutoka Arsenal kwa mkopo hadi mwishoni mwa msimu.
Arsene Wenger amesema uamuzi wa kumruhusu Kiungo huyo Chipukizi ni kumpa uzoefu wa Ligi Kuu.
-Okaka
Fulham wako hatua za mwisho kumchukua Straika kutoka AS Roma Stefano Okaka na kwa sasa anafanyiwa upimwaji afya ili ahamie Fulham kwa mkopo hadi mwishoni mwa msimu.
-Benjani
Meneja wa Sunderland Steve Bruce amethibitisha wako kwenye hatua za mwisho za mazungumzo na Wawakilishi wa Straika kutoka Zimbabwe Benjani Mwaruwaru ili wamnunue moja kwa moja kutoka Manchester City.

No comments:

Powered By Blogger