Friday 29 January 2010

Kitimtim cha Ligi Kuu
Bigi Mechi ni Jumapili wakati Arsenal wakiwa kwao Emirates watawavaa Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu Manchester United kwenye mechi inayozikutanisha Timu mbili zilizotenganishwa kwa pointi moja huku Man United wakiwa nafasi ya pili nyuma ya Chelsea na juu ya Arsenal walio nafasi ya 3.
Jumamosi kutakuwa na mechi 7 za Ligi Kuu na vinara wa Ligi Chelsea watasafiri kwenda kucheza na Burnley na Timu kubwa inayosuasua Liverpool itakuwa nyumbani kuwakaribisha Bolton Wanderers.
Aston Villa wanasafiri hadi London kucheza na Fulham huku wakiwa hawajashinda mechi zao 5 za mwisho za ugenini lakini Fulham wakiwa uwanja wa nyumbani Craven Cottage ni Timu ngumu.
Tottenham watakuwa nyumbani kucheza na Birmingham na huenda Mchezaji wao mpya Eidur Gudjohnsen akaonekana. Tottenham wako nafasi ya 4 wakiwa pointi 3 mbele ya Timu ya 5 Liverpool.
Hull City wataikaribisha Wolves na Timu hizi zote ziko eneo la hatari la kuporomoka Daraja na wanatofautiana kwa pointi moja tu kati yao.
Everton, ambao wameanza kupamba moto na hawajafungwa mechi 8 sasa, wanasafiri hadi Uwanja wa DW kucheza na Wigan ambao wanapigania uhai wao kwenye Ligi Kuu.
Nyumbani kwa West Ham, Uwanja wa Upton Park, kutakuwa na mechi kali kati ya wenyeji na Blackburn Rovers ambao wako nafasi ya 11 kwenye Ligi huku West Ham
wakielea nafasi ya 4 toka mkiani.
Jumapili, kabla ya Bigi Mechi ya Arsenal v Man United, Manchester City watataka kufuta machungu ya kubamizwa na Man United 3-1 siku ya Jumatano kwa kuisulubu Timu iliyo mkiani Portsmouth wakiwa Uwanja wa nyumbani City of Manchester.
RATIBA KAMILI:
[saa za bongo]
Jumamosi, 30 Januari 2010
[saa 12 jioni]
Birmingham v Tottenham
Fulham v Aston Villa
Hull v Wolves
Liverpool v Bolton
West Ham v Blackburn
Wigan v Everton
[saa 2 na nusu usiku]
Burnley v Chelsea
Jumapili, 31 Januari 2010
[saa 10 na nusu jioni]
Man City v Portsmouth
[saa 1 usiku]
Arsenal v Man United
Jumatatu, 1 Februari 2010
[saa 5 usiku]
Jumanne, 2 Februari 2010
[saa 4 dak 45]
Hull v Chelsea
Jumatano, 3 Februari 2010
Fulham v Portsmouth

No comments:

Powered By Blogger