Sunday 24 January 2010

Rooney awania kuvunja rekodi yake!!
Wayne Rooney anapigania kuivunja rekodi yake ya kufunga Magoli 23 kwa Msimu aliyoiweka huko nyuma na mpaka sasa ameshafunga Mabao 19 yakiwemo mabao manne aliyofunga jana kwenye mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Old Trafford dhidi ya Hull City.

Rooney, miaka 24, ametamka: “Ni mara yangu ya kwanza kufunga bao 4 kwenye mechi moja katika mpira wa kulipwa! Nataka nizipiku goli 23 nilizowahi kufunga Msimu mmoja na sasa nina goli 19 na bado mechi kama 20 hivi!”
Rooney akaongeza: “Tofauti Msimu huu ni kuwa naingia sana ndani ya boksi na nakuwepo kwenye nafasi za kufunga magoli!”
Hata Meneja wa Hull City, Phil Brown, amekiri: “Ni wazi ni Straika bora duniani! Ana uwezo wa kufunga ukimpa nusu upenyo tu! Hii ni hali nzuri kwa England kwenye Fainali za Kombe la Dunia!”
WAFUNGAJI BORA LIGI KUU:
1 Wayne Rooney Magoli 19
2 Jermaine Defoe 14
3 Didier Drogba 14
4 Darren Bent 14
5 Fernando Torres 12
6 Carlos Tevez 12
7 Louis Saha 11
8 Cesc Fabregas 11
9 Gabriel Agbonlahor 8
10 Carlton Cole, Arshavin, Berbatov, Cole, Kuyt Goli 7 kila mmoja

No comments:

Powered By Blogger