Thursday 1 April 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI:
Arsenal 2 Barcelona 2
Ni mechi waliyotawala Barcelona hasa kipindi cha kwanza na kama si ushujaa wa Kipa Manuel Almunia basi Barca wangekuwa mbele hata goli 5.
Lakini hadi mapumziko bao zilikuwa 0-0.
Kipindi cha pili kuanza tu, Shujaa Almunia akageuka kuwa mkosaji mkubwa pale alipotoka golini bila sababu ya msingi na kumpa mwanya Zlatan Ibrahimovic kumvika ‘kanzu’ na kupachika bao sekunde 30 tu tangu mpira uanze.
Alikuwa Ibrahimovic tena alieipa Barca bao la pili na kumfanya kila mtu ajue Barca wataondoka Emirates na lundo la migoli.
Lakini Arsene Wenger akafanya mabadiliko yaliyobadilisha mchezo pale alipomtoa Beki Bacary Sagna na kumuingiza Theo Walcott na Walcott hakufanya ajizi akaifungia Arsenal bao moja dakika ya 69 na kuwapa uhai.
Kwenye dakika ya 85, Refa Busacca akaipa Arsenal penalti baada ya kuamua Nahodha wa Barca Puyol alimchezea rafu Fabregas na pia kumpa Puyol Kadi Nyekundu.
Marudio ya tukio hilo yalionyesha ni uamuzi wa makosa.
Fabregas akafunga penalti hiyo na kuifanya ngoma iwe sare 2-2.
Timu hizi zitarudiana Nou Camp Aprili 6 huku Barcelona ikihitaji sare ya 0-0 au 1-1 ili ipite kwa vile wana magoli mawili ya ugenini.
Mechi hiyo ya marudio itachezwa huku kila Timu ikiwa haina Nahodha kwa vile Fabregas alipewa Kadi ya Njano ikiwa ni ya pili na Puyol alipata Kadi Nyekundu.
Vile vile Beki wa Barca Gerrard Pique ataikosa mechi hiyo kwa kupewa Kadi ya Njano ikiwa ni ya pili.
Hivyo, Barcelona watacheza mechi hiyo ya marudiano bila ya Masentahafu wao wa kawaida Puyol na Pique.
Vikosi vilivyoanza:
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Clichy, Song, Fabregas, Diaby, Nasri, Bendtner, Arshavin
Barcelona: Valdes, Dani Alves, Pique, Puyol, Maxwell, Messi, Keita, Busquets, Xavi, Pedro, Ibrahimovic.
Refa: Massimo Busacca [Switzerland]
Inter Milan 1 CSKA Moscow 0
Ndani ya San Siro, Mshambuliaji Milito aliipa Inter Milan ushindi wa bao 1-0 alipofunga goli hilo dakika ya 65 ya Kipindi cha Pili.
Timu hizi zitarudiana huko Moscow Aprili 6.
Vikosi vilivyoanza:
Inter Milan: Julio Cesar, Maicon, Materazzi, Samuel, Zanetti, Stankovic, Cambiasso, Eto’o, Sneijder, Pandev, Milito.
CSKA Moscow: Akinfeev, Vasili Berezutsky, Alexei Berezutsky, Ignashevich, Shchennikov, Krasic, Aldonin, Semberas, Mamaev, Honda, Necid.
Refa: Howard Webb [England]

1 comment:

Anonymous said...

NAKUPONGEZA KWA UNAZI WAKO. NINGESHANGAA SANA KAA UNGEISIFU ARSENAL. YAANI MPAKA MTU KAVUNJIKA MGUU LAKINI BADO UNADIRIKI KUSEMA KUWA KAPEWA PENATI KIMAKOSA! KUWA MCHAMBUZI WACHA UANCHESTER KWENYE UCHAMBUZI

Powered By Blogger