Tuesday 25 May 2010

SHAKIRA NA 'TIME FOR AFRICA', 'WIMBO WA TAIFA KOMBE LA DUNIA' BONDENI!! [Bofya hapa kwa Taarifa Zaidi]

Barca yapiga domo tu bila ofa ya Fabregas!!
Barcelona imesema wameongea na Arsenal na kuwafahamisha nia yao ya kutaka kufanya mazungumzo ili wamnunue Cesc Fabregas lakini hamna ofa yeyote iliyotolewa.
Fabregas aliiambia Arsenal wiki iliyokwisha nia yake ya kurudi Barca Timu aliyoanzia kucheza mpira akiwa mtoto kabla kujiunga na Arsenal.
Hata hivyo dalili zinaonyesha Arsenal hawatamwachia kirahisi Nahodha wao.
Mkurugenzi Mkuu wa Barcelona, Joan Oliver, amesema: “Bado hatujatoa ofa ila tumewajulisha nia yetu kufanya mazungumzo. Hatuna haraka.”
Nae Baba yake Mzazi Fabregas, Francesc Fabregas, amesema mjadala wa Arsenal na Barca utachukua muda mrefu kwa vile ishu yenyewe ni ngumu.
Baba huyo amekiri kuwa wao siku zote wanaishukuru Arsenal kwa kumkomaza Cesc kutoka Mtoto hadi kuwa Mwanaume kamili.
Fabregas ana Mkataba na Arsenal hadi 2012.
Ufaransa yataja Kikosi cha mwisho cha Wachezaji 23
Kocha wa Ufaransa Raymond Domenech ametangaza Kikosi chake cha Wachezaji 23 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia na majina hayo ndiyo yatawasilishwa FIFA Juni 1.
Ufaransa, iliyokuwa na Wachezaji 24 kambini, ilipata pigo pale Kiungo Lassana Diarra alipoumia na Domenech amesema haongezi Mtu na Kikosi kilichobaki ndicho cha mwisho na kitaenda Kombe la Dunia.
Kikosi kamili:
Makipa: Hugo Lloris (Olympique Lyon), Steve Mandanda(Olympique Marseille), Cedric Carrasso (Girondins Bordeaux)
Walinzi: Bacary Sagna (Arsenal), Patrice Evra (Manchester United), William Gallas (Arsenal), Eric Abidal (Barcelona), Sebastien Squillaci (Sevilla), Marc Planus (Girondins Bordeaux), Gael Clichy(Arsenal), Anthony Reveillere (Olympique Lyon)
Viungo: Alou Diarra(Girondins Bordeaux), Jeremy Toulalan (Olympique Lyon), Florent Malouda (Chelsea), Yoann Gourcuff (Girondins Bordeaux), Abou Diaby (Arsenal), Franck Ribery (Bayern Munich)
Mafowadi: Thierry Henry (Barcelona), Nicolas Anelka (Chelsea), Andre-Pierre Gignac (Toulouse), Sidney Govou (Olympique Lyon), Djibril Cisse (Panathinaikos), Mathieu Valbuena (Olympique Marseille)

No comments:

Powered By Blogger