Friday 28 May 2010

Daktari wa Argentina: Soka na Ngono Ruksa!!!
• Maradona kukimbia uchiii!!!
Daktari wa Timu ya Argentina ya Kombe la Dunia, Dr. Donato Vallani, amesema Wachezaji wa Timu hiyo ruksa kupata unyumba na Mapatna wao wa kawaida wakiwa huko Afrika Kusini kwenye Fainali za Kombe la Dunia.
Dr. Vallani amesema: “Wachezaji wako huru kufanya ngono na Wake zao na Wachumba zao! Wao si Viumbe toka Dunia nyingine! Lakini si kufanya hivyo saa 8 za usiku wakinywa pombe na kuvuta Sigara!”
Daktari huyo pia amesema Wachezaji ruksa kula Nyama Choma na glasi ya mvinyo ambavyo hupendwa sana huko Argentina lakini kukata Kilaji kwa kupindukia hairuhusiwi.
Argentina wanategemewa kutua Afrika Kusini leo na wapo Kundi B pamoja na Nigeria, Korea Kusini na Ugiriki.
Nigeria ndio wapinzani wa kwanza wa Argentina hapo Juni 12.
Wakati huo huo, Kocha wao Diego Maradona ameahidi kukimbia uchi katikati ya Jiji la Buenos Aires, Argentina endapo Nchi hiyo itatwaa Kombe la Dunia.
Maradona alikuwa Nahodha wa Argentina Mwaka 1986 walipochukua Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger