Sunday 23 May 2010

Mourinho yuko njiani kwenda Real!!
Kocha wa Inter Milan Jose Mourinho, ambae jana aliweka historia ya kuchukua Trebo, yaani kunyakua Vikombe vitatu kwa mpigo katika Msimu mmoja vikiwa ni Ubingwa wa Serie A, Coppa Italia na Klabu Bingwa Ulaya, amesema Real Madrid itakuwa nyumba yake ya tatu akimaanisha ataondoka Inter.
Jana Mourinho aliingia kwenye historia ya kuwa Meneja wa tatu kutwaa Ubingwa wa Ulaya akiwa Klabu mbili tofauti baada ya Diego Milito kupiga bao mbili na kuwaliza Bayern Munich na kuwafanya Inter wanyakue Kombe la UEFA CHAMPIONS LIGI.
Mourinho amesema: “Inter ni kwangu kama ilivyokuwa Chelsea. Ilikuwa ngumu kuhama Chelsea na nikihama Inter ni ngumu lakini hayo ni maisha, ndio Soka! Nilikuwa na nyumba mbili, Chelsea na Inter na sasa ntakuwa nay a tatu-Real Madrid!”
Alipoulizwa kwa nini anavutiwa na Real, Mourinho alijibu: “Ndio Klabu pekee inayonitaka!”

No comments:

Powered By Blogger