Saturday 29 May 2010

Cameroun 1 Slovakia 1
Mechi za majaribio kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia kwa Cameroun zimezidi kuwa ngumu baada ya leo tena kulazimisha sare ya 1-1 walipocheza na Slovakia ambao pia wako kwenye Fainali hizo wakishiriki kwa mara ya kwanza.
Hii ni mechi ya pili kwa Cameroun kutoka sare baada ya kwenda suluhu 0-0 na Georgia majuzi.
Katika mechi hii ya leo iliyochezwa Nchini Austria, Slovakia ndio walikuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 6 kwa mzinga wa Mita 18 wa Kamil Kopunek.
Cameroun, wakicheza bila ya Samuel Eto’o aliepumzishwa, walisawazisha kupitia kwa Eyong aliefunga dakika 7 kabla mchezo kwisha.
Cameroun wapo Kundi E kwenye Kombe la Dunia pamoja na Denmark, Japan na Uholanzi.
Mechi inayofuata ya majaribio kwa Cameroun ni Juni 1 huko Covilha, Ureno watakapoikwaa Ureno ambayo pia iko matayarishoni kwa Kombe la Dunia, kisha watacheza na Serbia Juni 5 huko Belgrade.

No comments:

Powered By Blogger