Friday 28 May 2010

Majaribio ya Waamuzi Watano kwa Mechi……………..
UEFA imeongeza muda wa kutumia Marefa Watano katika kila mechi na Msimu ujao yatahusisha pia Mashindano ya Klabu ya UEFA CHAMPIONS LIGI na yale ya Mataifa ya EURO 2012 baada ya kuanza kutumika Msimu uliopita kwenye EUROPA LIGI.
Mtindo huo wa Marefa Watano hutumia Marefa Watatu wa kawaida, yaani Refa Mkuu anaekuwa katikati Uwanjani akisaidiwa na Washika Vibendera Wawili wakiwa pembezoni ya Uwanja, huku nyuma ya kila mstari wa goli huwepo Refa Msaidizi mwingine mmoja na kufanya jumla ya Waamuzi kuwa Watano.
Bodi ya Kimataifa ya Vyama vya Soka [IFAB=The International Football Association Board] ambao ndiyo yenye mamlaka ya kubadili sheria za Soka Duniani na inayoundwa na Waawakilishi toka FIFA, Vyama vya Soka vya England, Scotland, Wales na Ireland, Vyama ambavyo ndivyo Waanzilishi wa Soka Duniani, ilibariki kutumika kwa mtindo wa Marefa Watano kwa mechi kwa UEFA na Vyama vingine vya Soka Duniani.
Mwezi Machi, IFAB iligoma kupitisha mapendekezo ya kutumika utaalam wa kisasa wa elektroniki kwenye mistari ya magoli ili kuwasaidia Marefa kuamua kama mpira umevuka mstari na hivyo ni goli au la.
Lakini mtindo huo wa Marefa Watano uliojaribiwa kwenye EUROPA LIGI Msimu uliopita ulipokewa kwa hisia tofauti na Makepteni wa Timu zilizoshiriki EUROPA LIGI ambao walipiga kura kupitia Chama chao cha Wachezaji wa Kulipwa, Fifpro, na Asilimia 70 waliona hamna kilichosaidia kwa kutumika Marefa Watano katika mechi moja.
Lakini UEFA wana mtizamo tofauti na wameona IFAB kubariki kutumika Mtindo huo na kuendelezwa kwa Majaribio kuhusisha UEFA CHAMPIONS LIGI na EURO 2012 ni kuukubali.
Nae Refa wa zamani wa Ligi Kuu England, Graham Poll, anahisi kubadili mfumo wa utumiaji Marefa una matatizo na alisema kuna wakati Marefa hao Watano kwa mechi moja walifanya kazi nzuri na akatoa mfano Dirk Kuyt alipoifungia goli Liverpool kwenye mechi na Benfica na Refa Msaidizi [Mshika Kibendera] akaashiria ni Ofsaidi lakini Refa Msaidizi mwingine aliekuwa nyuma ya goli, aliona Mchezaji aliekuwa ofsaidi hakuugusa na wala hakuingilia mchezo na hivyo ni goli halali na Refa Mkuu akalikubali.
Graham Poll akatoa mfano mwingine uliohusu Marefa Watano kwenye mechi ya EUROPA LIGI ya Fulham ambao, kwa pamoja, walifanya makosa makubwa ya kutaka kumtoa kwa Kadi Nyekundu Mchezaji ambae si mkosaji na ikabidi yule Mchezaji mkosaji akiri yeye ndie mwenye kosa na si yule alietaka kutolewa.
Poll amesema: “Siku zote makosa ya Kibanadamu yapo hata ukiweka Marefa wangapi! Lazima tukubali hilo au tuseme hatutaki na kutumia teknolojia!”
Matokeo Mechi za Kirafiki:
Alhamisi, 27 Mei 2010
Belarus 2 v Honduras 2
Denmark 2 v Senegal 0
South Africa 2 v Colombia 1

No comments:

Powered By Blogger