Tuesday 25 May 2010

England 3 Mexico 1
Wakicheza mechi yao ya kwanza ya kujipima nguvu tangu waweke kambi Nchini Austria kwa ajili ya Kombe la Dunia wiki moja iliyopita, England waliweza kuilaza Mexico, ambayo nayo pia iko Fainali za Kombe la Dunia, kwa bao 3-1.
Hadi mapumziko, England walikuwa mbele kwa bao 2-1.
Bao la kwanza la England lilifungwa dakika ya 17 baada ya kona ya Gerrard kumkuta Crouch aliepiga kichwa na kumfikia Ledley King aliemalizia kwa kichwa.
Bao la pili alifunga Peter Crouch baada kichwa cha Wayne Rooney kupanguliwa na Kipa Perez na mpira kugonga mwamba wa juu na kumbabatiza Crouch mkononi na kutinga wavuni.
Mexico walipata bao lao Mfungaji akiwa Franco kwenye dakika ya 48 baada ya kona.
Kipindi cha pili Mexico walimwingiza Mchezaji mpya wa Manchester United, Javier Hernandez aka Chicharito, kuchukua nafasi ya Franco alieumia.
England walifunga bao la 3 dakika mbili baada ya kipindi cha pili kuanza baada ya Beki wa Kulia, Glen Johnson, kupanda na kuachia fataki iliyopinda hadi wavuni.
Vikosi vilivyoanza:
England: Green, Glen Johnson, Ferdinand, King, Baines, Walcott, Gerrard, Carrick, Milner, Crouch, Rooney.
Akiba: Hart, James, Carragher, Dawson, Upson, Warnock, Lennon, Parker, Huddlestone, Wright-Phillips, Adam Johnson, Heskey, Defoe
Mexico: Perez, Juarez, Aguilar, Marquez, Salcido, Osorio, Torrado, Rodriguez, Giovani, Franco, Vela.
Akiba: Ochoa, Michel, Barrera, Castro, Blanco, Hernandez, Moreno, Guardado, Magallon, Torres, Bautista, Medina, Jonathan.
MATOKEO MECHI ZA KIRAFIKI:
Jumatatu, Mei 24
Argentina 5 v Canada 0 
Australia 2 v New Zealand 1
England 3 v Mexico 1
Japan 0 v Korea Kusini 2
Ureno 0 v Cape Verde 0
Afrika Kusini 1 v Bulgaria 1
RATIBA MECHI ZA KIRAFIKI:
Jumanne, Mei25
[saa za bongo]
Armenia v Uzbekistan [saa 12 jioni]
Georgia v Cameroun [saa 1 usiku]
Greece v Korea Kaskazini [saa 3 usiku]
Montenegro v Albania [saa 3 na robo usiku]
Nigeria v Saudi Arabia
Republic of Ireland v Paraguay [saa 3 dak 45 usiku]
Ukraine v Lithuania [saa 1 usiku]

No comments:

Powered By Blogger