Thursday 27 May 2010

Ni rasmi, Brazil kucheza Bongo!!!
Taifa Bora kwa Soka Duniani na ambao wanashika rekodi ya kutwaa Kombe la Dunia kwa kujitwika nalo mara 5, Brazil, watacheza mechi za kirafiki na Zimbabwe Juni 2 na Juni 7 watakuwa Dar es Salaam kucheza na Taifa Stars.
Mikataba kwa ajili ya mechi hizo mbili tayari imeshasainiwa na tayari Timu hiyo iko Afrika Kusini ilipowasili jana ikitokea kwao Brazil.
Rais wa TFF, Leodegar Tenga, akithibitisha ujio wa Brazil, alitamka kwa furaha: “Unazungumzia Timu Bora Duniani. Hii ni njia bora ya kuitangaza Nchi yetu. Na hii ni moja ya hatua tunazopasa kuchukua kukuza Soka letu. Italeta furaha Nchini na kuwapa moyo Vijana wetu.”
Brazil wataanza kampeni yao kwenye Kombe la Dunia Juni 15 kwa kucheza na Korea Kaskazini na wapo Kundi moja pamoja na Ivory Coast na Ureno.

No comments:

Powered By Blogger