Wednesday 26 May 2010

FIFA kupima Wachezaji 256 kabla Fainali Kombe la Dunia
FIFA itawapima Wachezaji wanane toka kila Timu katika Nchi zote 32 zilizo Fainali za Kombe la Dunia kabla Fainali hizo kuanza huko Afrika Kusini Juni 11.
Jumla ya Wachezaji 256 watapimwa mkojo na damu kabla ya Fainali ili kuchunguza kama wanatumia madawa yaliyopigwa marufuku.
Pia, wakati wa Fainali hizo, Wachezaji wawili toka kila Timu watapimwa baada ya kila mechi katika mechi zote 64 za Fainali za Kombe la Dunia.
Fainali za Kombe la Dunia zimekuwa tulivu bila Wachezaji kugunduliwa kutumia madawa yaliyopigwa marufuku isipokuwa ile Fainali ya Mwaka 1994 wakati Diego Maradona wa Argentina alipogundulika akitumia mchanganyiko wa madawa marufuku na akatimuliwa kwenye Fainali hizo.

No comments:

Powered By Blogger