Wednesday 26 May 2010

Brazil kutua Bongo njiani kwenda Bondeni?
[BOFYA KWA HABARI ZAIDI]

Pellegrini afukuzwa Real Madrid
Real Madrid imemtimua Kocha wake Manuel Pellegrini na kuiacha njia nyeupe kwa Kocha wa Inter Milan Jose Mourinho kuchukua wadhifa huo kama ilivyokuwa ikivumishwa.
Bodi ya Real ilikaa leo na kuto uamuzi wa kumtimua Pellegrini na Rais wake Florentino Perez ndie alietangaza maamuzi ya Bodi hiyo.
Huko Italia, Inter Milan wameshakata tamaa kumbakisha Mourinho na Rais wa Klabu hiyo Massimo Moratti ameshasema hategemei kama Kocha huyo machachari atabaki Inter.
Pellegrini alikuwa tayari amekalia kuti kavu huko Real baada ya Klabu hiyo kutumia zaidi ya Pauni Milioni 200 kuwanunua Mastaa kina Cristiano Ronaldo, Kaka, Karim Benzema na Xabi Alonso na mwishoni mwa Msimu kuambua patupu baada ya kuukosa Ubingwa wa la Liga, uliobebwa na Mahasimu wao FC Barcelona, kutupwa nja ya UEFA CHAMPIONS LIGI ambayo Fainali yake ilifanyika nyumbani kwa Real Uwanja wa Santiago Bernabeau na pia kubwagwa nje ya Copa del Rey na Timu ndogo sana na masikini sana.

No comments:

Powered By Blogger