Thursday 27 May 2010

Uholanzi 2 Mexico 1
Kwenye mechi ya kirafiki, Robin van Persie wa Holland alifunga bao mbili dhidi ya Mexico iliyopigwa 3-1 juzi Jumatatu na England huko Wembley, London.
Uholanzi, chini ya Kocha Bert van Marwijk ilicheza bila Mastaa Mark van Bommel, Arjen Robben, Wesley Sneijder na Nigel de Jong ambao wana maumivu kidogo.
Rafael van der Vaart, ambae dakika ya 8 alipiga fataki iliyogonga posti, alimtengenezea Van Persie kufunga bao la kwanza dakika ya 17 na dakika 3 baada ya mapumziko Van Persie akafunga bao la pili.
Katika dakika ya 74, Javier Hernandez, maarufu kama Chicharito, ambae ni Mchezaji mpya wa Manchester United, akaipatia Mexici bao lake moja.

No comments:

Powered By Blogger