Wednesday 26 May 2010

LISTI YA UBORA YA FIFA: Brazil Nambari Wani, Bongo bado nafasi ya 108!!!
Brazil wataanza Fainali za Kombe la Dunia huku wakiwa ndio Timu ya kwanza kwa Ubora kufuatia listi mpya ya FIFA.
Timu iliyo nafasi ya pili ni Spain wakifuatiwa na Ureno, Holland na Italy.
Katika Afrika Nchi iliyo juu kabisa ni Misri ambao wako nafasi ya 12. Katika Nchi za Afrika zilizo Fainali ya Kombe la Dunia Cameroun ndio wako juu kabisa wakiwa nafasi ya 19 na Wenyeji wa Kombe la Dunia Afrika Kusini wako nafasi ya 83.
Tanzania bado wameng’ang’ania nafasi ya 108.
Msimamo kwa Timu za juu ni:
1 Brazil
2 Spain
3 Portugal
4 Holland
5 Italy
6 Germany
7 Argentina
8 England
9 France
10 Croatia
11 Russia
12 Egypt
13 Greece
14 USA
15 Serbia
Mmiliki wa zamani Liverpool ajuta kuiuza!
David Moores amepasua kuwa anajuta sana kuiuza Liverpool kwa Wamarekani George Gillett na Tom Hicks na amewataka waiuze Klabu hiyo.
Moores aliiuza Liverpool Mwaka 2007 lakini Wamarekani hao wawili walioinunua wameitumbukiza Klabu kwenye Madeni makubwa.
Moores amewaambia: “Msiwaadhibu Washabiki! Uzeni Klabu!”
Gillett na Hicks walinunua Liverpool kwa Pauni Milioni 200 toka kwa Moores lakini utawala wao haukuwapendeza Washabiki na pia kuitumbukiza Klabu kwenye deni la zaidi ya Pauni Milioni 350 ndio kero kubwa ya Washabiki hao.
Pia kushindwa kwa Liverpool kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao kwa vile wamemaliza nafasi ya 7 kumewaudhi mno Wadau.
Gillett na Hicks walitangaza Mwezi Aprili kuwa wataiuza Liverpool lakini mpaka sasa hakuna Mnunuzi aliejitokeza.
Merida wa Ze Gunners atimkia Atletico
Kiungo wa Arsenal Fran Merida anarudi Spain baada ya kusaini Mkataba na Atletico Madrid akiwa Mchezaji huru.
Merida alikuwa Arsenal tangu 2006 aliposainiwa kutoka FC Barcelona lakini uchezaji wake ulikuwa wa nadra sana.
Straika Dindane ajiunga na Klabu ya Qatar
Straika wa Portsmouth Aruna Dindane amejiunga na Lekhwiya ya Qatar kwa Mkataba wa Miaka mitatu.
Dindane alikuwa Portsmouth kwa mkopo wa Mwaka mmoja akitokea Lens ya Ufaransa.
Klabu ya Lekhwiya pia imemsaini Bakary Kone toka kwa Mabingwa wapya wa Ufaransa Marseille.
Wote Dindane na Kone ni Wachezaji kutoka Ivory Coast na wamo kwenye Kikosi cha Nchi hiyo kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger