Thursday 27 May 2010

Yuko njiani Real, Mourinho awataka Cole, Maicon Real!!
Jose Mourinho, anaetegemewa kutangazwa kama Mrithi wa Manuel Pellegrini alietimuliwa jana ndani ya Masaa 24 yajayo, tayari ameshaanza kudokeza mikakati yake Real Madrid kwa kusema anataka akiwa hapo acheze mtindo wa kuwa na Mabeki wanne na kati yao Mafulbeki wawili wenye staili ya kupanda na kushambulia kama walivyo Ashley Cole, aliekuwa Mchezaji wake Chelsea, na Maicon ambae wako wote Inter Milan.
Kitu pekee kinachochelewesha Mourinho asitangazwe ndie Meneja mpya wa Real ni kipengele cha Mkataba wake kinachotaka Inter Milan walipwe Pauni Milioni 13.2 ikiwa Mkataba utakatizwa kabla ya mwisho wake Mwaka 2012.
Mourinho amenena: “Napenda kucheza na Mabeki wanne ingawa nimeshashinda mechi nyingi na Mabeki watatu. Kawaida nacheza na Difensi ya Mabeki wanne na wawili ni wale wa pembeni wanaopanda kushambulia kama wanavyofanya Maicon na Cole.”
Mourinho ndie aliemchota Ashley Cole kutoka Arsenal Mwaka 2006 kwenda Chelsea wakati alipokuwa Meneja wa Chelsea na kumtaja kwake Cole kumeleta hisia atamchukua Real akitua huko.
Mourinho pia alidokeza kuwa Frank Lampard na Steven Gerrard ni Wachezaji wanaofaa kwa Real.
MECHI ZA KIMATAIFA ZA KIRAFIKI
[saa za kibongo]
Alhamisi, 27 Mei 2010
Belarus v Honduras, [saa 1 na nusu usiku]
Denmark v Senegal, [saa 3 na robo usiku]
South Africa v Colombia, [saa 3 dak 35 usiku]
________________________________________
Ijumaa, 28 Mei 2010
Rep of Ireland v Algeria, [saa 3 dak 45 usiku]
________________________________________
Jumamosi, 29 Mei 2010
Azerbaijan v FYR Macedonia, [saa 12 jioni]
Congo DR v North Korea
Hungary v Germany, [saa 3 usiku]
Iceland v Andorra, [saa 4 usiku]
New Zealand v Serbia, [saa 12 na robo usiku]
Norway v Montenegro, [saa 11 jioni]
Poland v Finland, [saa 12 jioni]
Slovakia v Cameroon, [saa 9 mchana]
Spain v Saudi Arabia, [sa 1 usiku]
Sweden v Bosnia-Hercegovina, [saa 2 usiku]
Ukraine v Romania, [saa 2 na nusu usiku]
United Arab Emirates v Moldova, [saa 2 usiku]
USA v Turkey, [saa 3 usiku]
________________________________________
Jumapili, 30 Mei 2010
Belarus v South Korea, [saa 10 jioni]
Chile v Northern Ireland, [saa 5 usiku]
Japan v England, [saa 9 na robo mchana]
Mexico v Gambia, [saa 12 jioni]
Nigeria OFF Colombia, [saa 3 usiku]
Paraguay v Ivory Coast, [saa 3 usiku]
Tunisia v France, [saa 3 usiku]
Venezuela v Canada, [saa 8 na nusu usiku]
________________________________________
Jumatatu, 31 Mei 2010
Chile v Israel, [saa 11 alfajiri]
South Africa v Guatemala, [saa 3 na nusu usiku]
________________________________________
Jumanne, 1 Juni 2010
Australia v Denmark, [saa 9 na nusu usiku]
Netherlands v Ghana, [saa 3 na nusu usiku]
Portugal v Cameroon, [saa 3 na nusu usiku]
Switzerland v Costa Rica, [saa 3 na robo usiku]

No comments:

Powered By Blogger