Sunday 23 May 2010

Inter Bingwa Ulaya!!!!!!
• Inter 2 Bayern 0
Diego Milito amedhihirisha yeye ndie Mfungaji Bora wa Inter Milan alipopachika bao 2 na kuwapa Inter Ubingwa wao wa kwanza wa Ulaya katika Miaka 45 walipoifunga Bayern Munich bao 2-0 katika Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI iliyochezwa Uwanja wa Santiago Bernabeau, Madrid, Spain.
Katika mechi hii, Bayern walionekana kuutawala mchezo lakini walishindwa kuipenya ngome iliyoongozwa na Lucio na dhahiri walionyesha kumkosa Franck Ribery.
Milito alifunga bao la kwanza dakika ya 35 na la pili dakika ya 70.
Bao la la kwanza la Inter lilianza kwa Kipa Julio Cesar aliepandisha mpira wa juu mbele na Diego Milito akaupoza kwa pasi ya kichwa kwa Sneijder na Sneijder hakuchelewesha akapenyeza pasi kwa Milito aliekuwa kachomoka kuingia ndani ya boksi na Straika huyo toka Argentina hakufanya ajizi akamchambua Kipa wa Bayern, Butt, na kutingisha wavu.
Bao la pili lilitokana na pande la Samuel Eto’o kumkuta Milito nje ya boksi na akawahadaa Van Buyten na Demichelis kisha kumdanganya Kipa Butt kwa shuti la kifundi.
Vikosi vilivyoanza:
Bayern Munich: Butt; Lahm, Badstuber, Van Buyten, Demichelis; Altintop, Van Bommel, Schweinsteiger, Robben; Olic, Muller.
Inter Milan: Cesar; Maicon, Lucio, Samuel, Zanetti; Cambiasso, Pandev; Eto’o, Sneijder, Chivu; Milito.
Refa: Howard Webb (England).

No comments:

Powered By Blogger