Monday 24 May 2010

Hatma ya Mourinho Masaa 24 yajayo
Jose Mourinho anategemewa kumjulisha Rais wa Inter Milan, Massimo Moratti, uamuzi wake wa kujiunga na Real Madrid katika Masaa 24 yajayo.
Licha ya kuwa na Mkataba na Inter Milan hadi Juni 2012, kuna kipengele kwenye Mkataba huo kinachomruhusu Mourinho kuhama kabla kwisha.
Msemaji wa Mourinho amethibitisha atakutana na Moratti ndani ya Masaa 24 ili kuwekana sawa.
Wakati kuna taarifa za Wakala wa Mourinho, Jorge Mendes, kuwa Mjini Madrid akikamilisha mambo huko Milan, Meya wa Milan, Letizia Moratti, ambae ni Shemeji yake Massimo Moratti, Rais wa Inter Milan, amewalaumu Wanahabari wa Italia kwa kuondoka kwa Mourinho.
Mama huyo Meya amelalamika: “Naomba Wanahabari wajaribu kumbembeleza Mourinho abaki kwani ni kosa lao! Anaondoka kwa sababu kwingineko Ulaya Waandishi hawapondi Watu ovyo!”

No comments:

Powered By Blogger