Thursday 27 May 2010

Essien kwa heri World Cup
Michael Essien hatacheza Fainali za Kombe la Dunia kwa vile hawezi kupona goti lake kabla ya mwisho wa Julai.
Essien, ambae ni Mchezaji wa Ghana, aliumia goti akichezea Nchi yake kwenye mechi za awali za Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mwezi Januari huko Angola na tangu wakati huo hajachezea hata Klabu yake Chelsea.
Fainali za Kombe la Dunia zitaanza huko Afrika Kusini Juni 11 na kumalizika Jula11.
Kila Nchi iliyo Fainali hizo inatakiwa kuwasilisha Kikosi chake cha Wachezaji 23 kwa FIFA ifikapo Juni 1.
Ghana wako Kundi D pamoja na Ujerumani, Australia na Serbia.
Chicharito apata Kibali kucheza Man United
Straika toka Mexico Javier Hernandez, Miaka 21, amepewa Kibali cha Kazi Nchini England cha kuichezea Manchester United na rasmi atahesabika kama Mchezaji wa Klabu hiyo Julai 1.
Hernandez, maarufu kama Chicharito, alichukuliwa na Man United Aprili kutoka Klabu ya Chivas Guadalajara ya Mexico lakini usajili wake ulitegemea kupata Kibali cha Kazi ambacho kilikuwa na utata kwa vile alikuwa hajafikisha kuchezea mechi Asilimia 75 za Nchi yake Mexico katika Miaka miwili iliyopita kama kanuni za Kazi zinavyotaka kwa Wachezaji Soka wa Kulipwa watokao nje ya Jumuia ya Ulaya.
Hivyo ilibidi Man United waombe Kibali hicho cha Kazi kwa kutuma Maombi spesheli yaliyosisitiza kuwa Kijana huyo ana kipaji pekee ambacho ni ngumu kupatika katika Nchi za Ulaya kwa dau waliomnunulia.
Jopo la FA ambalo linasimamia Vibali hivyo kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya England liliafikiana na ombi la Man United na kumruhusu Javier Hernandez aka Chicharito kuanza kuichezea Klabu yake mpya.
Chicharito siku ya Jumatatu iliyopita aliichezea Mexico Kipindi cha pili ilipocheza mechi ya kirafiki na England Uwanjani Wembley.
Jana Chicharito aliichezea tena Mexico walipokutana na Uholanzi na alifunga bao la Nchi yake katika mechi ambayo Holland waliifunga Mexico 2-1.
Katika Fainali za Kombe la Dunia, Mexico wapo Kundi A pamoja na Wenyeji Afrika Kusini, Ufaransa na Uruguay.

No comments:

Powered By Blogger