Tuesday 31 August 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Hodgson aiangukia Spain kuhusu Torres
Roy Hodgson ameibembeleza Spain isimchezeshe Straika wake wa Liverpool Fernando Torres katika Mechi ya Makundi ya EURO 2012 Wiki hii na Liechtnstein na pia mechi inayofuata ya kirafiki dhidi ya Argentina ili kumpumzisha na kumpa muda wa kutosha kuendelea na tiba ya goti lake chini ya usimamizi wa Wataalam wa Viungo wa Liverpool.
Meneja huyo wa Liverpool amemwomba Meneja wa Spain Vicente Del Bosque amwondoe Torres kwenye Kikosi cha Spain ili abakie Liverpool kutibu goti lake lililomsumbua Msimu wote uliokwisha.
Hodgson amesema Torres anahitaji muda zaidi na Madaktari wa Klabu hiyo la sivyo akichezeshwa mechi mfululizo ataathirika baadae kadri Msimu unavyoendelea.
Mpaka sasa Spain haijatoa tamko lolote kuhusu Torres.

No comments:

Powered By Blogger