Saturday 4 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Kocha Algeria ajiuzulu!
• Ni siku moja tu baada ya kwenda sare na Bongo!!!
Kocha wa Timu ya Taifa ya Algeria, Rabah Saadane, amejiuzulu wadhifa wake ikiwa ni siku moja tu baada ya kutoka sare 1-1 na Tanzania huko Algiers katika mechi ya Makundi kugombea kufuzu kuingia Fainali za Mataifa ya Africa 2012.
Saadane alishika Ukocha Miaka mitatu iliyopita na aliiwezesha Algeria kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini Mwezi Juni ikiwa ni mara yao ya kwanza baada ya Miaka 24.
Shirikisho la Soka la Algeria limetaja kujiuzulu kwa Saadane ni kutokana na matokeo ya jana na wao wamekubali matakwa yake.

No comments:

Powered By Blogger