Thursday 2 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

VIKOSI WACHEZAJI 25: Majina 25 Kila Timu yatangazwa!!
• Hargreaves ndani Man United!!
Jana kila Timu ya Ligi Kuu England, ikiwa siku ya mwisho ya usajili wa Vikosi vya Wachezaji 25, iliwasilisha kwa Wasimamizi wa Ligi Kuu Listi zao na Klabu ya Tottenham imemwacha Difenda mahiri Jonathan Woodgate huku Manchester United ikimteua Owen Hargreaves kuwa mmoja wa Wachezaji wao.
Woodgate na Hargreaves ni majeruhi wa muda mrefu.
Woodgate alionekana uwanjani mara ya mwisho Novemba 2009 na Hargreaves amecheza mechi moja tu katika Miaka miwili iliyopita baada ya kupasuliwa magoti yake yote mawili huko Marekani.
Katika Listi ya Arsenal hakuna hata Mwingereza mmoja mbali ya Theo Walcott na Jack Wilshere ambao ingawa hawapo Kikosini ila ni ruksa kucheza kwa kuwa wapo chini ya Umri wa Miaka 21.
Sheria mpya za Ligi Kuu zimeitaka kila Klabu iwasilishwe Majina ya Wachezaji 25 kabla ya Saa 1 usiku, saa za bongo, Septemba 1 na ndani ya Wachezaji hao 25, wanane ni lazima wawe ‘wamelelewa’ nyumbani, ikimaanisha ni lazima wawe wamesajiliwa England au Wales na kukaa kwa Miaka mitatu kwenye Klabu zao kabla hawajatimiza Miaka 21.
Lakini Klabu zimepewa uhuru kuchezesha idadi ya zaidi ya Wachezaji 25 ikiwa tu Wachezaji hao wa ziada wako chini ya umri wa Miaka 21 [Mchezaji anahesabiwa hajatimiza Miaka 21 ikiwa Januari 1 ya Mwaka wa Msimu anaocheza hajafikisha umri huo].
Arsenal wameitumia Sheria hiyo kwa kusajili Kikosi cha Wachezaji 20 tu badala ya 25 huku 7 wakiwa ni wale ‘waliolelewa’ nyumbani na 13 ni wale ‘vijeba’ huku Chipukizi Theo Walcott na Jack Shilshere, licha ya kutosajiliwa rasmi katika Kikosi, wako huru kuichezea Arsenal kwa vile hawajatimiza Miaka 21.
Nahodha wa Arsenal, Cesc Fabregas, amesajiliwa kama mmoja wa Wachezaji 7 ‘waliolelewa’ nyumbani kwa vile alikuwepo hapo kwa zaidi ya Miaka mitatu kabla hajatimiza Miaka 21.
Vikosi kamili vya TIMU VIGOGO:
Arsenal [Wachezaji 20]
WALIOLELEWA NYUMBANI:
-Nicklas Bendtner
-Denilson
-Johan Djourou
-Cesc Fabregas
-Vito Mannone
-Gael Clichy
-Alex Song
WENGINEO:
-Manuel Almunia
-Andrey Arshavin
-Marouane Chamakh
-Abou Diaby
-Emmanuel Eboue
-Lukasz Fabianski
-Laurent Koscielny
-Samir Nasri
-Tomas Rosicky
-Bacary Sagna
-Robin Van Persie
-Thomas Vermaelen
-Sebastien Squillaci
Chelsea – [Wachezaji 19]
WALIOLELEWA NYUMBANI:
-Ashley Cole
-John Terry
-Frank Lampard
-Ross Turnbull
WENGINEO:
-Petr Cech
-Branislav Ivanovic
-Michael Essien
-Ramires
-Yossi Benayoun
-Didier Drogba
-John Mikel Obi
-Florent Malouda
-Jose Bosingwa
-Yuri Zhirkov
-Paulo Ferreira
-Salomon Kalou
-Alex
-Nicolas Anelka
-Henrique Hilário
Liverpool- [Wachezaji 21]
WALIOLELEWA NYUMBANI:
-Brad Jones
-Glen Johnson
-Steven Gerrard
-Joe Cole
-Jamie Carragher
-Jay Spearing
-Stephen Darby
-Paul Konchesky
WENGINEO:
-Daniel Agger
-Fabio Aurélio
-Fernando Torres
-Milan Jovanovic
-Sotirios Kyrgiakos
-Maxi Rodríguez
-Dirk Kuyt
-Lucas Leiva
-Jose Reina
-Martin Skrtel
-Christian Poulsen
-Ryan Babel
-Raul Meireles
Manchester United- [Wachezaji 24]
WALIOLELEWA NYUMBANI
-Gary Neville
-Jonny Evans
-Rio Ferdinand
-Wes Brown
-Wayne Rooney
-Ryan Giggs
Michael Carrick
-Paul Scholes
-John O’Shea
-Darren Fletcher
-Darron Gibson
-Ritchie De Laet
-Michael Owen
WENGINEO
-Edwin Van Der Sar
-Bebé
-Patrice Evra
-Anderson
-Dimitar Berbatov
-Ji-Sung Park
-Nemanja Vidic
-Luis Valencia
-Tomasz Kuszczak
-Javier Hernández
-Owen Hargreaves
Ferdinand yuko fiti
Rio Ferdinand jana alicheza Mechi yake ya kwanza tangu aumie goti mazoezini huko Afrika Kusini kabla kuanza Fainali za Kombe la Dunia na hivyo kulikosa Kombe hilo.
Rio, Miaka 31, alicheza dakika 45 za kwanza za mechi ya Rizevu wa Manchester United dhidi ya Oldham na Kocha wa Timu hiyo ya Rizevu, Ole Gunnar Solskjaer, amethibitisha kuwa Mchezaji huyo yuko fiti kurejea Kikosi cha Kwanza.
Mechi za Man United zifuatazo ni ile ya Ligi Kuu Septemba 11 na Everton huko Goodison Park, Septemba 14 na Rangers kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI huko Old Trafford na kisha Ligi Kuu na Liverpool pia Uwanjani Old Trafford Septemba 19.
Katika mechi hiyo ya Rizevu, Anderson, ambae aliumia goti Mwezi Februari, alicheza kwa dakika zote 90 na Macheda, ambae pia alikuwa majeruhi, alicheza na kufunga bao la pili na la ushindi katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Oldham.

No comments:

Powered By Blogger