Wednesday 1 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Mtu mwenye kasi sana Duniani ataka kuchezea Man United!
Bingwa wa Mbio za Mita 100, Usain Bolt, ameelezea nia yake ya kucheza Soka kwenye Klabu aipendayo ambayo ni Manchester United.
Katika Kitabu cha maisha yake, Usain Bolt, Miaka 24, ameandika: “Ikitokea ntacheza Soka, nitasaini kwa Timu niipendayo Manchester United. Watu wanasema hilo haliwezekani laki wao hawajaniona nnavyocheza hivyo huwezi jua nini kitatokea. Ikiwa Sir Alex Ferguson ataniona kwenye zile mechi za hisani anaweza kushawishika naweza kumbadili Ryan Giggs.”
Bolt ameshawahi kufanya mazoezi mara kadhaa na Man United kwenye Kituo chao huko Carrington na ameshahudhuria Mechi nyingi huko Old Trafford.
VUVUZELA HAZITAKIWI ULAYA!
UEFA imepiga marufuku Vuvuzela katika Mashindano yote ya Ulaya baada ya ala hiyo kupata umaarufu Dunia nzima kufuatia Fainali za Kombe la Dunia zilizochezwa huko Afrika Kusini Mwezi Juni na Julai.
Klabu kadhaa za Ulaya tayari zimeshazipiga marufuku Vuvuzela kutotumika katika Viwanja vyao na sasa UEFA imezikataa kwenye Mashindano ya UEFA CHAMPIONS LIGI, EUROPA LIGI na Mechi za EURO 2012.

No comments:

Powered By Blogger