Saturday 4 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Algeria 1 Tanzania 1
Wakicheza ugenini, Uwanja wa Moustapha Tchaker huko Algiers, Taifa Stars ilienda sare ya 1-1 na Algeria, iliyosheheni Wachezaji toka Ligi za Ulaya, katika mechi ya kwanza ya Kundi lao ili kuwania kuingia Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika za Mwaka 2012.
Taifa Stars walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 33 kupitia Abdi Kassim ambae frikiki yake kali ilitinga kimiani.
Lakini Algeria, wakiongozwa na Masupastaa wa Ulaya, Hasan Yebda, Ziaya na wengineo, walisawazisha dakika ya 45 Mfungaji akiwa Adlene Guedioura.
Mechi inayofuata kwa Taifa Stars ni ya ugenini pia huko Morocco Oktoba 7.

No comments:

Powered By Blogger