Saturday 4 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

England yaichapa Bulgaria 4-0
• Rooney apika goli zote!
England imeanza kampeni yao ya kufuzu kuingia Fainali za EURO 2012 zitakazochezwa huko Poland na Ukraine kwa pamoja Mwaka 2012 kwa kuibamiza Bulgaria mabao 4-0 Uwanjani Wembley Jijini London katika Mechi ya Kundi G huku Jermaine akipachika bao 3 na Wayne Rooney kuzipika bao zote 4.
Jermaine Defoe alifunga mabao yake matatu dakika ya 3, 61 na 86.
Adam Johnson, alieingia kipindi cha pili badala ya Theo Walcott, alifunga bao lake dakika ya 83.
Katika Mechi nyingine ya Kundi G, Montenegro iliifunga Wales 1-0.
Mechi inayofuata kwa England ni Jumanne, Septemba 7 watakaposafiri kwenda kupambana na Timu ngumu Uswisi.
Vikosi vilivyoanza:
ENGLAND: Hart, G Johnson, Dawson, Jagielka, A Cole, Walcott, Milner, Barry, Gerrard, Defoe, Rooney.
BULGARIA: Mihailov, Ivanov, Milanov, Manolev, Iliyan Stoyanov, Yankov, Angelov, Stiliyan Petrov, Martin Petrov, Bojinov, Popov.
REFA: Viktor Kassai [Hungary]
VIGOGO WOTE ULAYA WASHINDA, FRANCE………!!!!
Wakati Vigogo wote wa Ulaya wakishinda mechi zao za kwanza za kuwania kuingia Fainali za EURO 2012, Ufaransa bado ni hali ile ile ya Kombe la Dunia walipofungwa nyumbani na Belarus kwa bao 1-0.
Bao la ushindi kwa Belarus lilifungwa dakika ya 86 na Kislyak.
EURO 2012 MATOKEO KAMILI:
Ijumaa, 3 Septemba 2010
Armenia 0 v Rep of Ireland 1
Kazakhstan 0 v Turkey 3
Andorra 0 v Russia 2
Moldova 2 v Finland 0
Faroe Islands 0 v Serbia 3
Montenegro 1 v Wales 0
Latvia 0 v Croatia 3
Romania 1 v Albania 1
Sweden 2 v Hungary 0
Lithuania 0 v Scotland 0
Luxembourg 0 v Bosnia-Hercegovina 3
Estonia 1 v Italy 2
Slovakia 1 v FYR Macedonia 0
Belgium 0 v Germany 1
Greece 1 v Georgia 1
Liechtenstein 0 v Spain 4
San Marino 0 v Netherlands 5
Slovenia 0 v Northern Ireland 1
England 4 v Bulgaria 0
France 0 v Belarus 1
Iceland 1 v Norway 2
Portugal 4 v Cyprus 4

No comments:

Powered By Blogger