Friday 26 February 2010

Adebayor kifungoni mechi 4
Straika wa Manchester City Emmanuel Adebayor atazikosa mechi zote za timu yake za mwezi Machi baada ya kufungiwa mechi 3 kwa kutolewa kwa Kadi Nyekundu kwa kumpiga Mchezaji wa Stoke kwenye mechi ya FA siku ya Jumatano walipofungwa 3-1 na adhabu hiyo moja kwa moja imeongezwa mechi moja kwa vile alishafungiwa mwezi Septemba kwa kero zake katika mechi ya Arsenal.
Adebayor atazikosa mechi za Manchester City na Chelsea, Sunderland, Fulham na Wigan.
SKANDALI LA TERRY: Sasa Bifu la Terry v Bridge!!!!!
Juzi Wayne Bridge alitangaza kujiuzulu kuichezea Timu ya Taifa ya England ili asigongane na John Terry anaetuhumiwa kutembea na gelfrendi wake ambae ni Mama wa Mtoto wake na sasa vita ya chini kwa chini ya Terry na Bridge imeibuka huku Wachezaji hao wakitazamiwa kupambana Uwanjani Stamford Bridge kwenye mechi ya Ligi Kuu kati ya Timu ya Bridge Manchester City na Timu ya Terry Chelsea siku ya Jumamosi.
Inadaiwa marafiki wa Terry wameanza kuzoza kuwa Bridge ni mwoga na ndio maana amejitoa Timu ya Taifa ya England.
Kocha wa England Fabio Capello akizungumzia kujitoa kwa Bridge alisema bado ana matumaini Mchezaji huyo anaweza akabadili mawazo na taimu bado ipo kumwita Kikosini ili acheze Fainali za Kombe la Dunia linaloanza Juni huko Afrika Kusini.
Wayne Bridge ndie mrithi wa dhahiri wa nafasi ya Beki wa kushoto Ashley Cole alieumia vibaya enka yake na itabidi Capello awafikirie Wachezaji Stephen Warnock wa Aston Villa na Leighton Baines wa Everton kuchukua nafasi hiyo.
Mchezaji mwingine ambae pengine agekuwa nambari wani kuchukua nafasi hiyo ni Kieran Gibbs wa Arsenal lakini nae kavunjika mfupa wa kidoleni mguuni.
Bridge, aliechezea England mara 36, alitoa tamko la kujiuzulu England kupitia Mawakili wake na alisema kujitoa kwake ni kwa sababu huu si wakati muafaka na kuwepo kwake kunaweza kuleta mgawanyiko Kikosini England.
Lakini, chinichini, inadaiwa Bridge na Terry waliongea kwa simu ili kutuliza sakata hilo linalowahusu lakini mazungumzo hayo yakaisha kwa simu kukatwa baada ya kutoafikiana.
Mechi ya Jumamosi huko Stamford Bridge kati ya Chelsea na Manchester City itafuatiliwa na wengi na kamera, bila shaka, zitalenga kuona kama Terry na Bridge watapeana mikono kabla kuanza mechi kama ilivyo kawaida.

No comments:

Powered By Blogger