Wednesday 24 February 2010

LIGI KUU: Man United 3 West Ham 0
Manchester United wameinyuka West Ham mabao 3-0 katika mechi pekee ya Ligi Kuu iliyochezwa Old Trafford Jumanne usiku na kuikaribia Chelsea inayoongoza Ligi wakiwa pointi moja nyuma yao.
Bao la kwanza lilianzishwa na Park, alieingia dakika ya 19 baada ya Anderson kuumia, kumpa Berbatov aliempasia haraka Valencia pembeni nae bila kusita alitia krosi kwa Rooney aliefunga kwa kichwa dakika ya 38.
Bao la pili pia lilitokana na krosi ya Valencia kumaliziwa kwa kichwa na Rooney kwenye dakika ya 55.
Michael Owen, alieingizwa dakika ya 78, alipachika bao la 3 dakika ya 80.
Mechi inayofuata kwa Manchester United ni Fainali ya Kombe la Carling Uwanjani Wembley hapo Jumapili watakapovaana na Aston Villa.
Vikosi:
Man Utd: Foster, Neville, Brown, Vidic, Evra, Valencia, Gibson, Scholes, Anderson [Park, 19], Berbatov [Owen, 78], Rooney [Diouf, 78].
Akiba: Kuszczak, Owen, Park, Rafael, Evans, Fletcher, Diouf.
West Ham: Green, Faubert, Tomkins, Upson, Spector, Behrami [Cllison, 63], Noble, Kovac, Diamanti, Franco [Mido, 46], Cole.
Akiba: Stech, Dyer, Ilan, Mido, Da Costa, Collison, Daprela.
Refa: Alan Wiley
UEFA CHAMPIONS LIGI:
Olympiakos 0 Bordeaux 1
Stuttgart 1 Barcelona 1
Ciani aliifungia Bordeaux bao moja na la ushindi wakiwa ugenini huko Ugiriki na kuichapa Olympiakos 1-0 katika mechi ya kwanza ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Timu hizi zitarudiana Machi 9 huko Ufaransa.
Nao Mabingwa Watetezi Barcelona wametoka sare ya 1-1 na Stuttgart ugenini huko Ujerumani na ni Ibrahimovic aliewapa droo hiyo baada ya kusawazisha bao dakika ya 52.
Stuttgart ndio walipata bao la kwanza dakika ya 25 Mfungaji akiwa Cacau.
Timu hizi zitarudiana Uwanja wa Nou Camp nyumbani kwa Barcelona Machi 9.
EUROPA LIGI: Benfica 4 Hertha Berlin 0
Benfica wameitandika Hertha Berlin ya Ujerumani 4-0 na kusonga mbele Raundi ya Mtoano ya Timu 16 kwa jumla ya mabao 5-1.
Mabao ya Benfica yalifungwa na Oscar Cardozo, bao 2, Pablo Aimar na Javi Garcia.
Timu hizi zilitoka sare 1-1 katika mechi ya kwanza wiki iliyopita.
Benfica watacheza na mshindi kati ya FC Copenhagen au Marseille raundi ijayo.
Mechi nyingine za EUROPA LIGI zitachezwa Alhamisi ili kukamilisha jumla ya Timu 16 kwenye raundi inayofuata ya mtoano.

No comments:

Powered By Blogger