Friday 26 February 2010

Portsmouth kuporomoka!!!
• Kukatwa Pointi 9!!!
Imethibitika Portsmouth ndio itakuwa Klabu ya kwanza ya Ligi Kuu England kuangukia kwenye mikono mibaya ya kuwa chini ya Msimamizi maalum ili kuepuka kutangazwa Mufilisi.
Portsmouth, ambayo msimu huu mmoja imebadili Wamiliki wanne, imeshindwa kupata Mnunuzi na Jumatatu iko Mahakamani kwenye kesi iliyofunguliwa na Mamlaka ya Kodi inayotaka Klabu hiyo ifilisiwe kwa kushindwa kulipa kodi.
Msimamizi huyo maalum atakuwa na kazi ya kurekebisha muundo wa uendeshwaji wa Klabu hiyo ili kuifanya iwe inavutia kwa Wanunuzi.
Lakini hatua hii ya kuiweka chini ya Msimamizi maalum kuinusuru isifilisiwe, ingawa ni hatua nzuri kwa uhai wa Klabu, ni kinyume cha sheria za Ligi Kuu na Klabu hiyo itakatwa pointi 9.
Portsmouth wapo mkiani mwa Ligi Kuu na wana pointi 16 tu na kukatwa pointi 9 ni wazi kunawahukumu washushwe Daraja mwishoni mwa msimu.

No comments:

Powered By Blogger