Saturday 27 February 2010

LIGI KUU: Pompey, Birmingham ushindi kwa tuta!!!
Pompey washinda ugenini!!!
Portsmouth wameyaondoa matatizo yao ya nje ya uwanja kwa kupata ushindi mtamu ugenini kwa kuipiga Burnley bao 2-1.
Portsmouth walipata bao la kwanza kupitia Frederic Piquionne lakini Burnsley wakasawazisha kwa bao la Martin Paterson.
Jamie O’Hara akaikosesha Pompey bao la pili pale alipokosa penalti kwa Kipa wa Burnley Brian Jensen kuokoa.
Lakini Pompey wakapata penalti ya pili baadae na safari hii ikapigwa na Mchezaji toka Algeria Hassan Yebda na akafunga bao la pili na la ushindi.
Portsmouth walimaliza mechi hii wakiwa Watu 10 baada ya Mchezaji wao Ricardo Rocha kupata Kadi Nyekundu kwenye dakika za majeruhi baada ya kulambwa Kadi za Njano mbili.
Birmingham 1 Wigan 0
Bao la penalti iliyopigwa na James McFadden dakika chache kabla haftaimu limeipa ushindi Birmingham wakiwa nyumbani dhidi ya Wigan.
Penalti hiyo ilitolewa baada ya Beki wa Wigan Mario Melchiott kumkata ngwala Keith Fahey ndani ya boksi.
Mwishoni mechi hii iliongezwa dakika 7 kufidia muda iliposimama baada ya Msaidizi wa Refa, mshika kibendera, Trevor Massey, kuumizwa na kupasuliwa kichwani na kibendera cha kona kilichompiga baada ya Beki wa Birmingham Ridgewell kumkata McCarthy na kukivaa kibendera hicho kilichoruka.
Bolton 1 Wolves 0
Mlinzi Zat Knight aliuondoa ukame wa magoli wa Bolton uliodumu zaidi ya masaa 9 pale alipofunga goli dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza baada ya pande tamu la mwenzake Chung-Yong Lee.
Kipindi cha pili, Wolves walikosa bao za wazi kadhaa zikiwemo mbili zilizogonga posti.

No comments:

Powered By Blogger