Monday 22 February 2010

Mourinho, Chelsea hawana siri!!
Jose Mourinho anajiamini anajua jinsi Chelsea itakavyocheza siku watakapokutana na Timu yake ya sasa Inter Milan kwenye mpambano wa UEFA CHAMPIONS LIGI hapo Jumatano ijayo Februari 24 Uwanjani San Siro.
Hivi karibuni, Mourinho alikwenda Stamford Bridge kuishuhudia Chelsea ilipocheza mechi ya Ligi Kuu na Fulham na kushinda 2-1.
Mourinho, aliekuwa Meneja wa Chelsea kwa miaka mitatu na kushinda Vikombe vitano kabla kuondoka Septemba 2007, amedai hakuna kitu kilichobadilika tangu aondoke.
Mourinho amedai: “Nilipokwenda Stamford Bridge nilitazama kila kitu! Kabla ya mechi bado wanapasha miili joto kama walivyokuwa wakifanya walipokuwa chini yangu! Niliona wakijihami kutoka frikiki kama vile tulivyokuwa tukifanya! Mara nyingine hucheza fomesheni ya 4-4-2 yenye umbo la almasi wakishambulia, mara nyingine 4-3-3 na hiyo ni sawa kabisa na mifumo tuliyokuwa tukitumia!”
Mourinho ameendelea kudai kuwa kwa vile Ancelotti amebakisha vitu vingi alivyokuwa akifanya yeye bila kuleta mabadiliko makubwa ndio maana Timu imetulia na ina mafanikio kwa sasa.
Mourinho ameongeza kwa kusema Chelsea haina siri kwake na Timu ina watu wapya Anelka na Ivanovic tu na waliobaki kina Cech, Carvalho, Terry, Cole, Essien, Mikel, Drogba, Malouda, Joe Cole na Kalou ni Vijana wake.
Mourinho ametamka: “Chelsea hawana siri kwangu! Mimi kama Kocha sina siri kwao!”
Je Mourinho na Chelsea ya Ancelotti nani mbabe?
Mancini ataka Tevez arudi haraka kuokoa jahazi!!
Carlos Tevez ambae yuko kwao Argentina kwa matatizo ya kifamilia kwa siku 9 sasa na kuzikosa mechi 3 za Timu yake Manchester City ametakiwa arudi haraka na Bosi wake Roberto Mancini ili kuokoa jahazi.
Man City jana walitoka suluhu 0-0 na Liverpool kwenye Ligi Kuu na kukosekana kwa Carlos Tevez kulionekana wazi wazi kwenye mechi hiyo.
Jumatano, Man City wanarudiana na Stoke City kwenye mechi ya Raundi ya 5 ya FA Cup na Jumamosi wana kindumbwendumbwe na Chelsea huko Stamford Bridge kwenye Ligi Kuu.
Man City kwa sasa wako nafasi ya 5 kwenye Ligi Kuu na wanapigania nafasi ya 4 ili wafuzu kucheza UEFA msimu ujao lakini zipo Timu 4 zilizotenganishwa na pointi moja tu zinazogombea nafasi hiyo.
Timi hizo ni:
-Tottenham [walio nafasi ya 4] wana pointi 46 [kwa mechi 27]
-Man City pointi 46 [mechi 26]
-Liverpool pointi 45 [mechi 27]
-Aston Villa pointi 45 [mechi 26]
Mancini amekiri kumkosa Tevez ni matatizo makubwa kwao na wanapigana kumrudisha haraka Manchester ili angalau awahi mechi ya Jumamosi na Chelsea.
Owen akata tamaa kuitwa Kombe la Dunia!!
Straika wa Manchester United Michael Owen ameanza kukata tamaa kuhusu kuwemo kwenye Kikosi cha England cha Fainali za Kombe la Dunia.
Owen, miaka 30, amesema: “Ni muda mrefu tangu nichezee England. Huwezi kukata tamaa kuchezea tena lakini inaelekea nafasi yangu ni finyu!”
Wakati Kocha wa England Fabio Capello amekuwa akitilia mkazo kwamba Wachezaji wa England ni wale fiti tu na wanaocheza kila mara Kikosi cha kwanza cha Klabu zao, Owen ameweza kuanza mechi 5 tu za Klabu yake Man United za Ligi Kuu na kufunga goli 2 na amefunga bao 5 katika mechi nyingine.
Mechi pekee Owen aliyocheza na kutia fora ni ile ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE alipofunga bao zote 3 katika ushindi wa Man United wa 3-1 dhidi ya Wolfsburg.
England watacheza mechi ya kirafiki Machi 3 na Misri huko Wembley na Capello atateua Kikosi chake wikiendi hii inayokuja.
Pia Capello anatakiwa ateue Kikosi cha awali cha Kombe la Dunia cha Wachezaji 35 kabla ya Mei 12 na ikifika Juni 1 Kikosi cha watu 23 lazima kifikishwe FIFA tayari kwa Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 10 huko Afrika Kusini.
Capello pia anakabiliwa na utata mkubwa kuhusu uteuzi wa Mchezaji Wayne Bridge ambae ndie mrithi wa wazi wa Beki wa kushoto Ashley Cole alie majeruhi lakini kuna skandali kubwa la John Terry alievuliwa Unahodha wa England kwa kashfa ya kutembea na gelfrendi wa Wayne Bridge.
Je wawili hao, Terry na Bridge, wanaweza kucheza pamoja Difensi ya England?
KANDANDA LA WIKI:
Jumanne, Februari 23
LIGI KUU
[saa 5 usiku]
Man United v West Ham
UEFA CHAMPIONS LIGI
Olympiakos v Bordeaux
VfB Stuttgart v Barcelona
EUROPA LIGI
Benfica v Hertha Berlin
Jumatano, 24 Februari 2010
UEFA CHAMPIONS LIGI
CSKA Moscow v Sevilla
Inter Milan v Chelsea
Alhamisi, Februari 25
EUROPA LIGI:
Sporting Lisbon v Everton
Hapoel Tel aviv vFC Rubin Kazan
Juventus vAjax
Valencia v Club Brugge
Wolfsburg v Villareal
Red Bull Salzburg v Standard Liege
Werder Bremen v FC Twente
Fenerbahce v Lille
Anderlecht v Athletic de Bilbao
Olympique de Marseille v FC Kobenhavn
AS Roma v AS Roma
Galatasaray vAtletico de Madrid
Shakhtar Donetsk v Fulham
FC Unirea Urziceni v Liverpool
PSV Eindhoven v Hamburger SV
Jumamosi, February 27
LIGI KUU
[saa 9 dak 45 mchana]
Chelsea v Man City
[saa 12 jioni]
Birmingham v Wigan
Bolton v Wolves
Burnley v Portsmouth
[saa 2 na nusu usiku]
Stoke v Arsenal
Jumapili, Februari 28
LIGI KUU
[saa 10 jioni]
Tottenham v Everton
[saa 12 jioni]
Liverpool v Blackburn
Sunderland v Fulham
FAINALI CARLING CUP
[saa 12 jioni]
Manchester United v Aston Villa

No comments:

Powered By Blogger