Sunday 21 February 2010

Villa yaitandika Burnley 5-2
Ndani ya Villa Park, Aston Villa wameichabanga Burnley 5-2 katika mechi ya pili ya Ligi Kuu leo Jumapili.
Burnley ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao baada ya gonga zao tamu kuichana difensi ya Villa na Fletcher kufunga kirahisi.
Villa walisawazisha kwa bao la Ashley Young ambalo shuti lake lilipenya katikati ya miguu ya Madifenda wa Burnley na kuparaza miguu yao na kutikisa wavu.
Hadi mapumziko bao zilikuwa 1-1.
Ndipo kipindi cha pili mvua ya magoli ikaanguka kwa bao 2 za haraka za Stewart Downing na kuifanya Villa iwe mbele 3-1.
Emile Heskey akafunga la 4 na Agbonlahor akapachika bao la 5 huku Paterson akiifungia Burnley bao lao la pili.
Van der Sar kurefusha mkataba
Kipa wa Manchester United Edwin van der Sar atasaini mkataba mpya utakaomuweka Old Trafford hadi 2011 baada ya mkataba wake wa sasa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.
Van der Sar, miaka 39, amesema: “Nataka kuendelea kucheza hivyo ntasaini mkataba mpya. Klabu inataka nibaki na nina furaha hapa. Bado niko fiti!”
Kipa huyo ambae aliwahi kuzichezea Ajax na Juventus amekuwa na msimu mgumu safari hii na kuzikosa baadhi ya mechi kwanza alipoumia kidole halafu goti na wakati huo huo Mkewe akaugua ghafla na ikabidi arudi kwao Uholanzi kumuuguza.

No comments:

Powered By Blogger