Tuesday 23 February 2010

LIGI KUU LEO: Man United v West Ham
Leo saa 5 usiku, saa za bongo, Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu, Manchester United watajimwaga uwanjani nyumbani Old Trafford kuivaa West Ham katika mechi pekee ya Ligi Kuu.
Katika mechi yao ya mwisho ya Ligi, Man United walifungwa na Everton huko Goodison Park mabao 3-1.
West Ham walishinda mechi yao ya mwisho walipoipiga Wigan bao 3-0.
Leo Man United huenda wakawa na Madifenda wao wa kati, Rio Ferdinand na Nemanja Vidic, ambao hawajacheza pamoja kwa vile wote walikuwa majeruhi lakini Ferdinand alipopona na kucheza mechi yake ya kwanza akaadhibiwa na kufungiwa mechi.
Katika mechi yao ya kwanza ya Ligi huko Upton Park, Man United ilishinda bao 4-0.
Vikosi leo vitatokana na:
Man United: Van der Sar, Neville, Brown, Rafael, Ferdinand, Vidic, Evans, Fabio, Park, Anderson, Valencia, Carrick, Scholes, Fletcher, Obertan, Gibson, Rooney, Owen, Berbatov, Diouf
West Ham: Green, Stech, Spector, Faubert, Upson, Tomkins, Da Costa, Daprela, Parker, Behrami, Kovac, Collison, Noble, Diamanti, Stamislas, Cole, Mido, Ilan, Franco, McCarthy
Refa: Alan Wiley
Ancelotti achochea mechi ya Inter Milan v Chelsea
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti amechochea moto mbele ya pambano lao na Inter Milan huko San Siro, Milan, Italia la hapo kesho la UEFA CHAMPIONS LIGI kwa kudai kuwa Italia yote inataka Jose Mourinho ashindwe.
Mvutano wa Mourinho na Anceotti ni wa tangu Ancelotti alipokuwa Bosi AC Milan ambao ni Mahasimu wakubwa wa Inter Milan.
Mourinho ana uhusiano mbovu na Makocha wengine wa Klabu za Serie A pamoja na Viongozi wa Chama cha Soka cha Italia kufuatia kubatuka ovyo kwake na hilo limempa kichwa Carlo Ancelotti adai Italia nzima inataka Mourinho na Timu yake Inter Milan washindwe.
Ancelotti ameliambia Gazeti moja la Italia kuwa ‘Italia yote, ukiondoa Mashabiki wa Inter Milan, watakuwa wakiisapoti Chelsea hapo kesho!’
Ancelotti pia amemponda Mourinho kwa kujigamba kuwa alipoondoka yeye Chelsea hamna mtu alieleta Kikombe huko Stamford Bridge.
Ronaldo wa Brazil kung’atuka 2011
Ronaldo ametangaza kuwa mwakani atastaafu kucheza soka.
Ronaldo, ambae ameshanyakua Kombe la Dunia mara mbili akiwa na Brazil, amesema: “Nishaamua- miaka hii miwili ni ya mwisho!”
Ronaldo, miaka 33, kwa sasa anachezea Soka lake huko kwao Brazil akiwa na Klabu ya Corinthians na pia ameshachezea Klabu za Ulaya kama vile PSV Eindhoven, Barcelona, Inter Milan, Real Madrid na AC Milan.
Ameichezea Timu ya Brazil mara 97 na kufunga bao 62 na kunyakua nayo Kombe la Dunia mwaka 1994 na 2002.
Katika Fainali za Kombe la Dunia yeye ndie mwenye rekodi ya kufunga bao nyingi na ana jumla ya mabao 15.
Ronaldo ameshashinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa FIFA mwaka 1996, 1997 na 2002. Ameshinda Ballon D’or, Tuzo inayoashiria Mchezaji Bora Ulaya, mwaka 1997 na 2002.
Ronaldo katika miaka ya hivi karibuni amekuwa na matatizo makubwa ya kuumia hasa goti na pengine hilo ndilo limemfanya aamue kujiuzulu.

No comments:

Powered By Blogger