Saturday 27 February 2010

Nigeria yamteua Msweden Lagerback Kocha
Nigeria imemteua aliekuwa Kocha wa Sweden Lars Lagerback kuwa Kocha wa Timu ya Taifa yao ambayo ipo Fainali Kombe la Dunia.
Mara baada ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika huko Angola mwezi Januari walikofika Nusu Fainali, Nigeria walimtimua kazi Kocha wao Shuaibu Amodu licha ya kuwaingiza Fainali Kombe la Dunia.
Lagerback alikuwa Kocha wa Sweden lakini alijuzulu baada ya Sweden kushindwa kufuzu kuingia Fainali Kombe la Dunia.
Lagerback amepewa mkataba wa miezi mitano ambao utamuwezesha kuwepo kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini ambapo Nigeria wapo Kundi moja na Argentina, Ugiriki na Korea ya Kusini.
Majina ya vigogo waliohusishwa na kazi ya Ukocha Nigeria ni pamoja na Glenn Hoddle, Sven Goran Eriksson na Bruno Metsu.
SAKATA LA POMPEY: Msimamizi spesheli atua, asema Grant anabaki!!!
Msimamizi Maalum wa kuinusuru Portsmouth isifilisiwe, Andrew Andronikou, ameshatua Klabuni hapo na licha ya kuahidi kuisafisha Klabu hiyo pia amethibitisha Meneja Avram Grant atabaki Klabuni hapo hadi mwishoni mwa msimu na pia hakutakuwa na uuzwaji wa Wachezaji wa chapuchapu ili kupata fedha.
Portsmouth inakisiwa kuwa na deni la Pauni Milioni 60 na Jumatatu ipo Mahakama Kuu kwenye kesi ambayo Mamlaka ya Kodi iliitaka Mahakama hiyo iitangaze Klabu hiyo imefilisika kwa sababu ilishindwa kulipa kodi lakini kwa vile Klabu hiyo ipo chini ya Msimamizi Maalum uamuzi wa kuifilisi utaondolewa na Mahakama hiyo.
Hata hivyo, Portsmouth inakabiliwa na adhabu ya kukatwa pointi 9 na Ligi Kuu kwa vile imekiuka taratibu kwa kuwa mikononi mwa Msimamizi na adhabu hii, ukichukua hali ya Pompey kuwa mkiani ikiwa na pointi 17 tu, ni lazima itaishusha Daraja.
Andrew Andronikou ametamka: “Hamna kuuza Wachezaji chapuchapu! Lakini, ninahitaji mtaji wa kufanyia kazi hivyo tutaongea na Ligi Kuu tupate kibali cha kuuza Mchezaji mmoja au wawili!”
Andronikou atasaidiwa kwenye kazi yake hiyo na Peter Kubik na amesema kazi yake ya kwanza ni kutathmini nini kimeharibika na baada ya wiki 8 atakutana na Wadai wote.
Msimamizi huyo amewaomba Mashabiki wote wa Pompey kuisaidia Klabu hiyo na kuendelea kuisapoti katika mechi zilizobaki za msimu huu.

No comments:

Powered By Blogger