Saturday 27 February 2010

KIJANI & DHAHABU: Mashabiki Man United wajizatiti kuwang’oa kina Glazer!
Kikundi cha Mashabiki wa Manchester United, wanaojiita ‘MUST’ [Manchester United Supporters Trust], kimetangaza kuwa kimeiteua Kampuni ya ushauri ya kwenye mtandao ambayo ilishiriki uchaguzi wa Marekani na kufanikisha ushindi wa Obama mtandaoni, ili kuongeza nguvu kampeni yao na kupata Masapota watakaofikia idadi ya Watu 100,000 ili kuing’oa Familia ya Glazer katika umiliki wa Manchester United.
Mashabiki hao wa Man United, wanaovaa rangi za kijani na dhahabu hizi zikiwa ndizo rangi za kwanza za Newton Heath Timu anzilishi ya Man United na hiyo ikiwa ishara yao ya upinzani, kwa sasa wanakadiriwa kufikia Watu 52,000.
Kwenye Fainali ya Carling Cup Jumapili huko Wembley, Manchester United watakapocheza na Aston Villa, wimbi la kijani na dhahabu linategemewa kutanda miongoni mwa Mashabiki wa Man United ikionyesha kupamba moto kwa upinzani huo.

No comments:

Powered By Blogger