Wednesday 24 February 2010

Leo marudio FA Cup
Mechi za Raundi ya 5 ya FA Cup ambazo Timu zilitoka sare zinarudiwa leo na mechi hizo ni:
-Stoke City v Man City
-Aston Villa v Crystal Palace
-Tottenham v Bolton
Washindi wa mechi za leo wanasonga Robo Fainali ya Kombe hili.
Vidic afurahi kurudi tena dimbani, Rio mashakani!
Hajacheza mechi yeyote tangu 2010 ianze kwa kuandamwa na maumivu lakini jana Beki wa Manchester United Nemnja Vidic alikuwepo uwanjani Old Trafford na kuisaidia Timu yake kifunga West Ham bao 3-0 katika mechi ya LigI Kuu.
Mwenyewe Vidic amefurahia kupona kwake na amebashiri kuwa ingawa Man United iko nyuma ya Chelsea kwenye msimamo wa Ligi lakini wao wana imani Ubingwa ni wao tena.
Ingawa Man United wanafurahia kurudi kwa Vidic lakini huenda wakamkosa tena Difenda wao mkubwa Rio Ferdinand ambae alishindwa kucheza mechi ya jana na West Ham baada ya tatizo lake la mgongo kumrudia tena na huenda akaikosa Fainali ya Kombe la Carling na Aston Villa hapo Jumapili.
Mourinho atabiri ngoma ngumu leo!!
Jose Mourinho, aliewahi kuwa Kocha wa Chelsea na sasa yuko Inter Milan, ametabiri kuwa pambano la leo ni gumu mno na halitabiriki.
Inter Milan na Chelsea leo zinakutana huko San Siro katika mechi ya kwanza ya UEFA CHAMPIONS LIGI na marudio yake ni Machi 9 huko Stamford Bridge.
Mourinho amesema licha ya yeye kuijua nje ndani Chelsea hilo haliisaidii Inter Milan kushinda mechi hiyo na akatoa mfano alipokuwa na Chelsea walicheza na FC Porto Timu yake ya zamani lakini hilo halikumsaidia kuishinda FC Porto na badala yake walishinda moja na kufungwa moja.
Vile vile Mourinho alisema Carlo Ancelotti, Kocha wa Chelsea, hanufaiki na chochote kwa kuijua Inter Milan nje ndani kwa vile tu alikaa na Wapinzani wao wakubwa AC Milan na maisha yote kuishi Italia.
Nae Ancelotti amekanusha yale madai kuwa alitoa matamshi kwamba Italia yote haitaki Mourinho na Inter Milan kushinda na akasema mechi ya Jumatano ni ngumu na haitabiriki.

No comments:

Powered By Blogger