Friday 26 February 2010

EUROPA LIGI: Everton nje, Fulham, Liverpool zapeta!!
Timu za Fulham na Liverpool, zikicheza ugenini, zilipata matokeo mazuri na hivyo kusonga mbele kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 lakini wenzao Everton walichapwa mabao 3-0 huko Ureno mikononi mwa Sporting Lisbon na hivyo kubwagwa nje ya EUROPA LIGI.
Huko Ukraine, Fulham walitangulia kupata bao dakika ya 33 lakini Shakhtar Donetsk walisawazisha dakika ya 69 na mechi ikaisha 1-1.
Shakhtar Donetsk ndio walikuwa wameshinda Kombe la UEFA msimu uliopita na Kombe hilo sasa linaitwa EUROPA LIGI.
Fulham walishinda mechi ya kwanza 2-1 na hivyo kufuzu kwa jumla ya mabao 3-2.
Katika mechi hiyo Danny Murphy wa Fulham alipewa Kadi Nyekundu dakika ya 90 kwa kumpiga teke Mchezaji wa Donetsk.
Huko Romania, Liverpool waliichapa Unirea Urziceni mabao 3-1 na kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-1.
Unirea ndio waliopata bao la kwanza kupitia Joao Bruno Fernandes lakini Javier Mascherano wa Liverpool akasawazisha.
Ryan Babel na Steven Gerrard wakaongeza bao mbili na kuwafanya Liverpool wakutane na Lille ya Ufaransa Raundi ijayo ya Mtoano.
Huko Ureno mabao ya Sporting Lisbon yaliyofungwa na Miguel Veloso, Pedro Mendes na Fernandez yamewabwaga nje Everton kwa jumla ya mabao 3-2.
Everton walishinda mechi ya kwanza 2-1.
MATOKEO Mechi za Marudiano
Alhamisi, Februari 25
Anderlecht 4 v Athletci Bilbao 0 [jumla mabao 5-1]
Fenerbahce 1 v Lille 1 [2-3]
Galatasaray 1 v Atletico Madrid 2 [2-3]
Hapoel Tel Aviv 0 v Rubin Kazan 0 [0-3]
Juventus 0 v Ajax 0 [2-1]
Marseille 3 v FC Copenhagen 1 [6-2]
PSV 3 v Hamburg 2 [3-3, Hamburg wamefuzu kwa magoli ya ugenini]
Roma 2 v Panathinaikos 3 [4-6]
SV Red Bull Salzburg 0 v Standard Liege 0 [4-6]
Shakhtar Donetsk 1 v Fulham 1 [2-3]
Sporting Lisbon 3 v Everton 0 [4-2]
Unirea Urziceni 1 v Liverpool 3 [1-4]
Valencia 3 v Club Brugge 0 [3-1]
Werder Bremen 4 v FC Twente 1 [4-2]
Wolfsburg 4 v Villareal 1[6-3]
RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16
Alhamisi, Machi 11
Juventus v Fulham
Atletico Madrid v Sporting Lisbon
Valencia v Werder Bremen
Hamburg v Anderlecht
Benfica v Marseille
Lille v Liverpool
Panathinaikos v Standard Liege
Rubin Kazan v Wolfsburg
[MECHI ZA MARUDIANO MACHI 18]

No comments:

Powered By Blogger