Sunday 21 February 2010

Blackburn 3 Bolton 0
Katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu leo Jumapili, Blackburn wameipiga Bolton mabao 3-0 huku barafu ikidondoka mtindo mmoja kipindi cha pili.
Blackburn walipata bao la kwanza kabla ya haftaimu mfungaji akiwa Nicola Kalinic baada ya kupokea pasi toka kwa Junior Hoilett.
Kipindi cha pili Jason Roberts na Gael Givet waliongeza mabao ya Blackburn na kuifikisha nafasi ya 12 wakiwa na pointi 34.
Bolton wako nafasi ya pili toka mkiani wakiwa na pointi 23.
Maskini Pompey!!
Waliongoza 1-0 kwa bao la Piquionne dakika ya 35 lakini Portsmouth, Timu iliyo matatizoni nje na ndani ya uwanja wakikabiliwa na ukata na wako mkiani kwenye Ligi Kuu, ilijikuta ikitandikwa 2-1 nyumbani kwao Fratton Park hapo jana Jumamosi kwenye mechi ya Ligi.
Robert Huth aliisawazishia Stoke City dakika ya 50 na Stoke wakapata pigo pale Mchezaji wao Andy Wilkinson alipopewa Kadi mbili za Njano na hivyo kutolewa kwa Kadi Nyekundu lakini ni wao walioshinda baada ya Mchezaji wao wa akiba Salif Diao kupachika bao la pili dakika ya 91.
Kwa ushindi huo, Stoke wako nafasi ya 11 wakiwa na pointi 34 na Portsmouth bado wako nafasi ya 20 ikiwa ya mwisho na wana pointi 16 tu.
KWINGINEKO ULAYA: Matokeo
BUNDESLIGA
Ijumaa, Februari 19
1899 Hoffenheim 2 v Borussia Moenchengladbach 2
Jumamosi, Februari 20
Nurnberg 1 v Bayern Munich 1
Borussia Dortmund 4 v Hannover 1
Hamburg 0 v Eintracht Frankfurt 0
Mainz 05 0 v Bochum 0
Cologne 1 v Stuttgart 5
SERIE A
Jumamosi, Februari 20
Inter Milan 0 v Sampdoria 0
Genoa 3 v Udinese 0
LA LIGA
Jumamosi, Februari 20
Deportivo La Coruna 2 v Xerez 1
Real Mallorca 1 v Sevilla 3
Barcelona 4 v Racing Santander 0

No comments:

Powered By Blogger