Saturday 20 February 2010

Fergie: “Tumepigwa vibaya!!”
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson mara baada ya Timu yake kupokea kipigo cha mabao 3-1 huko Goodison Park toka kwa Everton amekubali Timu yake imetandikwa vibaya na inawasikitisha.
Ferguson alisema: “Tumepigwa vibaya, huo ndio ukweli! Imenisikitisha na Wachezaji wanasikitika! Wao ni binadamu na wanachezea Manchester United na hawapendi kufungwa! Lakini tumefungwa hapa!”
Nae Meneja wa Everton David Moyes amedai kuwa sasa Everton haiogopi mtu na inaweza kuifunga Timu yeyote.
Katika mechi mbili mfululizo, Everton imezifunga Timu za juu za Ligi Kuu baada ya kuitandika Chelsea 2-1 na kisha Man United 3-1.
Everton wako nafasi ya 8 kwenye msimamo wa Ligi na wana pointi 38.
Chelsea ndie anaeongoza akiwa na pointi 61, Man United wa pili pointi 57 na Arsenal ni wa 3 akiwa na pointi 55.

No comments:

Powered By Blogger