Wednesday 17 February 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: AC Milan 2 Man United 3
Ingawa mechi hii iltawaliwa kidogo na AC Milan lakini Manchester United ndio wameibuka kidedea kwa kushinda kwa mabao 3-2 huu ukiwa ushindi wao wa kwanza hapo San Siro katika mechi 4 walizocheza na AC Milan Uwanjani hapo.
AC Milan ndio walioanza mechi hii kwa kishindo kwa mkwaju wa Ronaldinho kumbabatiza Michael Carrick na kumbabaisha Kipa Van der Sar na kutinga wavuni ikiwa ni dakika ya 3 tu ya mchezo.
Scholes alisawazishia Man United dakika ya 36 na hadi mapumziko bao zilikuwa 1-1.
Mabao mawili ya vichwa ya Wayne Rooney kwenye dakika ya 66 na 74 yalifanya ngoma iwe 3-1 lakini kazi nzuri ya Ronaldinho ilimaliziwa na Clarence Serdorf aliefunga bao la pili kwa Milan dakika ya 85.
Katika dakika za majeruhi Kiungo wa Man United Michael Carrick alipata Kadi ya Pili ya Njano na hivyo kupewa Nyekundu na kutolewa na sasa ataikosa mechi ya marudiano hapo Machi 10.
Vikosi vilivyoanza:
AC Milan: Dida, Bonera, Nesta, Thiago Silva, Antonini, Beckham, Pirlo, Ambrosini, Ronaldinho, Alexandre Pato, Huntelaar.
Akiba: Abbiati, Gattuso, Inzaghi, Seedorf, Flamini, Favalli, Abate.
Man Utd: Van der Sar, Rafael Da Silva, Ferdinand, Jonathan Evans, Evra, Nani, Carrick, Scholes, Fletcher, Park, Rooney.
Akiba: Kuszczak, Neville, Brown, Owen, Berbatov, Valencia, Gibson.
Refa: Olegario Benquerenca (Portugal)
UEFA CHAMPIONS LIGI: Lyon 1 Real Madrid 0
Bao la Jean Makoun limeiwezesha Lyon kuifunga bao 1-0 Timu kigogo Real Madrid katika mechi iliyochezwa Ufaransa.
Timu hizi zitarudiana huko Uwanja wa Bernabeau, Madrid, Spain Machi 10.
LIGI KUU: Stoke City 1 Man City 1
Katika mechi pekee ya Ligi Kuu iliyochezwa Jumanne huko Britannia Stadium mtu 10 Stoke City walipata sare ya 1-1 na Manchester City.
Timu hizi zilikutana juzi kwenye Kombe la FA na kutoka sare na watarudiana tena Februari 24 kupata mshindi atakaeingia Robo Fainali ya Kombe hilo.
Stoke City, wakicheza pungufu baada ya Difenda Abdoulaye Faye kupewa Kadi Nyekundu kwa kumwangusha Adebayor wakati akiwa mtu wa mwisho.
Lakini, huku wakiwa watu 10, Stoke ndio walipata bao la kuongoza kupitia Glenn Whelan.
Man City walisawazisha kwa bao la Gareth Barry aliepokea mpira wa kichwa kutoka kwa Adebayor.
Kwa sare hii, Man City wameipiku Liverpool na kuchukua nafasi ya 4 wakiwa pointi moja mbele ya Liverpool na huku wana mechi moja mkononi.
EUROPA LIGI: Everton 2 Sporting Lisbon 1
Everton wameichapa Sporting Lisbon ya Ureno mabao 2-1 katika mechi ya kwanza ya EUROPA LIGI iliyochezwa Goodison Park huko Liverpool.
Mabao ya Everton yalifungwa na Steven Pienaar na Distin.
Sporting Lisbon walipata bao lao kwa penalti iliyosababisha pia Difenda wa Everton Distin apewe Kadi Nyekundu na penalti hiyo kufungwa na Miguel Veloso.

No comments:

Powered By Blogger