Monday 15 February 2010

Man United safarini Milan!!!
Nemanja Vidic na Anderson hawakuwamo kwenye Kikosi cha Wachezaji 22 wa Manchester United waliosafiri leo kutoka Manchester kwenda Milan, Italia kwa pambano la kesho huko San Siro na AC Milan la UEFA CHAMPIONS LIGI.
Wachezaji hao wanasemekana bado ni majeruhi.
Mchezaji mwingine aliebaki Jijini Manchester ni Mkongwe Ryan Giggs ambae amevunjika mkono.
Nani na Rio Ferdinand ambao wanatumikia vifungo vya mechi 3 na 4 kila mmoja huko England wamo Kikosini na vifungo vyao havihusu mechi za Ulaya na hivyo wanaweza kucheza kesho.
Kikosi kamili kilichosafiri: Van der Sar, Foster, Kuszczak; Neville, Brown, J Evans, Ferdinand, Fabio, Rafael, Evra; Valencia, Park, Nani, Obertan, Scholes, Fletcher, Carrick, Gibson; Rooney, Berbatov, Owen, Diouf.
LIGI KUU kuanzisha michuano maalum kuipata Timu ya 4 kucheza UEFA!!
Vigogo wapinga!!
Ligi Kuu England ipo mbioni kutaka kuanzisha michuano maalum ili kuipata Timu ya nne itakayocheza UEFA CHAMPIONS LIGI badala ya ule mtindo wa sasa wa Timu 4 za juu zinazomaliza Ligi kwenda moja kwa moja UEFA CHAMPIONS LIGI.
Mpango huo mpya utafanya Timu 3 tu za juu ndizo ziingie moja kwa moja UEFA na Timu zitakazomaliza nafasi ya 4 hadi ya 7 zicheze michuano maalum ili kuipata Timu moja itakayojumuika na hizo Timu 3 za juu.
Nia ya kuanzisha michuano hiyo maalum ni kuleta ushindani mkubwa kwenye Ligi Kuu baada ya kuwa inatawaliwa na Timu 4, nazo ni Chelsea, Manchester United, Arsenal na Liverpool, miaka nenda rudi.
Mpango huo wa michuano maalum umeungwa mkono na Timu zote isipokuwa vigogo hao wanne.

No comments:

Powered By Blogger