Saturday 20 February 2010

Droo Kombe la Mataifa Afrika 2012 tayari!!
Katika Droo iliyofanyika leo, Bongo imepangwa Kundi la 4 pamoja na Algeria, Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati katika mechi za mtoano kupata Timu zitakazocheza Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2012 zitakayofanyika katika Nchi za Gabon na Equatorial Guinea ambao watakuwa Wenyeji wa pamoja.
Makundi yapo 11 na Mshindi wa kila Kundi pamoja na Timu za pili 3 za Makundi zilizo na matokeo bora ndizo zitajumuika na Wenyeji hao wawili katika Fainali hizo na kufanya jumla ya Nchi 16.
Togo haikuwekwa kwenye Droo hiyo kwani inatumikia kifungo cha kutokucheza Mashindano mawili ya Kombe hilo walichopewa na CAF kwa kujitoa Fainali zilizochezwa mwezi Januari huko Angola.
Togo, waliojitoa baada ya Basi lao kupigwa risasi na kuuliwa watu watatu, wamekata rufaa Mahakama ya Usuluhishi Michezoni ambayo imeshaiambia CAF kuwa endapo Togo watashinda rufaa yao itabidi waingizwe kwenye michuano ya Afrika.
Mechi hizi za Makundi zitaanza Septemba mwaka huu.
MAKUNDI:
KUNDI 1: Mali, Cape Verde Islands, Zimbabwe, Liberia
KUNDI 2: Nigeria, Guinea, Ethiopia, Madagascar
KUNDI 3: Zambia, Mozambique, Libya, Comoros Islands
KUNDI 4: Algeria, Morocco, Tanzania, Central African Republic
KUNDI 5: Cameroon, Senegal, DR Congo, Mauritius
KUNDI 6: Burkina Faso, Gambia, Namibia, Mauritania
KUNDI 7: Egypt, South Africa, Sierra Leone, Niger
KUNDI 8: Ivory Coast, Benin, Rwanda, Burundi
KUNDI 9: Ghana, Congo, Sudan, Swaziland
KUNDI 10: Angola, Uganda, Kenya, Guinea Bissau
KUNDI 11: Tunisia, Malawi, Chad, Botswana

No comments:

Powered By Blogger