Thursday 18 February 2010

Viera ana kesi FA!!
Kiungo wa Manchester City Patrick Viera amefunguliwa mashtaka ya kutumia mabavu kufuatia kumpiga teke Mchezaji wa Stoke City Glenn Whelan katika mechi ya Ligi Kuu siku ya Jumanne katika tukio ambalo Refa Alan Wiley hakulichukulia hatua na alibaki kuongea na Viera tu.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu kati ya Stoke na Man City uwanjani Britannia ilimalizika 1-1.
Baada ya mechi hiyo, Meneja wa Stoke, Tony Pulis, aliitaka FA ichunguze video za tukio hilo.
Akipatikana na hatia, Viera atafungiwa mechi 3 na atazikosa mechi za Timu yake Manchester City dhidi ya Liverpool, siku ya Jumapili, Stoke City ya FA Cup na ya Chelsea kwenye Ligi.
Viera, ambae aliichezea Arsenal kabla ya kwenda Italia, alishawahi kupewa Kadi Nyekundu mara 10 katika miaka 9 aliyokuwa Arsenal.
Viera amepewa muda mpaka Alhamisi jioni ili aweze kukata rufaa na Kamisheni ya Sheria itakaa Ijumaa kuamua shauri lake.
Mabosi wa Klabu wapinga michuano maalum kupata Timu ya 4 kucheza Ulaya!!!
Mara baada ya kuibuka habari kuwa FA inatafakari kuweka michuano maalum kwa Timu zitakazomaliza Ligi nafasi ya 4 hadi ya 7 kushindana ili kupata Timu moja itakayojumuika na Timu 3 za juu kucheza mashindano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE, Mabosi kadhaa wa Ligi Kuu nao wameibuka kupinga mpango huo.
Kwa taratibu za sasa Timu 4 za juu ndizo zinaingia moja kwa moja kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Majuzi, Meneja wa Everton, David Moyes, ameupinga mpango huo kwa kuusema hauna maana na unaleta msongamano bure wa mechi.
Nae Bosi wa Liverpool, Rafa Benitez, ameupuuza mpango huo na kusema utaupa mzigo zaidi Timu za Ligi Kuu ambazo zinakabiliwa na mechi nyingi kwa sasa.
Benitez amesema: “Hivi kuna faida gani kwa Timu inayomaliza nafasi ya 4 kucheza na Timu ya nafasi ya 7 ambayo pengine iko nyuma yake pointi 20?”
Benitez ameongeza kwa kusema kwa taratibu za sasa tayari Timu zina mechi nyingi na wanapata majeruhi wengi.

No comments:

Powered By Blogger