Friday 19 February 2010

LEO MIAKA 100 YA OLD TRAFFORD
Miaka 100 iliyokwisha, tarehe 19 Februari 1910, Uwanja wa Old Trafford ulifunguliwa rasmi kwa mechi kati ya Manchester United na Liverpool ambayo Liverpool walishinda 4-3 mbele ya Watazamaji 45,000.
Uwanja huu kwa sasa unaweza kuchukua Watazamaji 75,957 na ni wa pili kwa ukubwa baada ya Wembley Stadium huko England.
Old Trafford ulibatizwa jina la “Theatre of Dreams”, yaani “Jukwaa la Ndoto” na Sir Bobby Charlton aliekuwa Mchezaji wa zamani mahiri wa Manchester United na England.
Mwaka 1909, Mwenyekiti wa Manchester United, John Henry Davies, alitoa Pauni Elfu 60 toka mfukoni mwake mwenyewe na kuujenga Uwanja huo.
Siku hiyo Februari 19, 1910, Kikosi cha kwanza kabisa kuchezea Manchester United kilikuwa: Harry Moger; George Stacey, Vince Hayes; Dick Duckworth, Charlie Roberts, Sam Blott; Billy Meredith, Harold Halse, Tom Homer, Sandy Turnbull, George Wall.

No comments:

Powered By Blogger