Sunday 14 February 2010

DROO YA ROBO FAINALI FA CUP:
Mara baada ya mechi ya mwisho ya Raundi ya 5 ya Kombe la FA hivi leo imefanyika Droo ya mechi za Robo Fainali ambazo zinatakiwa zichezwe Machi 6 na 7.
RATIBA NI [Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]:
Chelsea v Man City au Stoke City
Fulham v Bolton au Tottenham
Reading au West Brom v Crystal Palace au Aston Villa
Portsmouth v Birmingham
FA Cup: Palace 2 Villa 2
Goli la dakika ya 87 la Petrov limeiokoa Aston Villa kutupwa nje ya Kombe la FA na hivyo kupata suluhu 2-2 huko Selhurts Park nyumbani kwa Timu Mufilisi Crystal Palace ambayo ni taabani kifedha.
Timu hizi sasa zitarudiana Villa Park Febrruari 24 kupata mshindi atakaeingia Robo fainali.
FA Cup: Fulham 4 Notts County 0
Fulham, wakiwa nyumbani Craven Cottage, wametinga Robo Failali ya Kombe la FA baada ya kuifumua Notts County manao 4-0.
Hadi mapumziko Fulham walikuwa mbele kwa bao 2-0 Wafungaji wakiwa Simon Davies na Bobby Zamora.
Kipindi cha pili, Damien Duff na Stefano Okaka wakaongeza bao 2 kwa Fulham.
Fujo baada ya mechi ya FA Cup jana!!
Mashabiki na Polisi walipambana mjini Southampton hapo jana mara baada ya Klabu ya Southampton kubamizwa 4-1 na jirani zao Portsmouth kwenye mechi ya Kombe la FA.
Fujo hizo za Mashabiki zilishamira nje ya Uwanja wa Mtakatifu Maria, Uwanja wa Southampton, huku matofali, chupa na viti vikirushwa kila upande na Polisi kulazimika kuwakamata Mashabiki kadhaa.
Mara nyingi Klabu hizi zilizo jirani zikikutana huwa kunatokea vurugu kati ya Mashabiki wao.
Jana Polisi walilazimika kufunga baa zote karibu ya Uwanja kwa masaa mawili ili kuzuia mlipuko wa fujo.

No comments:

Powered By Blogger